Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Wakazi wa mkoa wa Shinyanga wamesema Miaka 61 ya uhuru serikali inapaswa
kuongeza kasi ya kuleta maendeleo ili Mkoa uweze kufanana na rasilimali
zilizopo.
Wamesema licha ya kufikiwa kwa mafanikio mbalimbali
lakini Mkoa wa Shinyanga umedumaa kimaendeleo ikilinganishwa na rasilimali
zilizopo ikiwemo Mifugo, kilimo cha mazao ya biashara pamoja na madini ya almas
Wameyasema hayo leo kwa nyakati tofauti wakati
wakizungumza na Misalaba Blog kama
sehemu ya maadhimisho ya Miaka 61 ya uhuru ambapo wameomba serikali iongeze
kasi ya uboreshaji wa huduma za kijamii kwenye eneo la miundombinu.
Wakati huo huo Mwenyekiti wa usalama barabarani Mkoa
wa Shinyanga (RSA) Seif Nasolo amewapongeza viongozi viongozi wa Mkoa na Wilaya
kwa kusikiliza na kutatua kero za wananchi hali ambayo imesaidia au kuondoa
changamoto mbalimbali zilizopo katika jamii.
Hata hivyo baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Shinyanga wameahidi kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Dkt. Jomaary Satura katika uboreshaji wa miundombinu mbalimbali hali ambayo inaleta madhari nzuri ya Mji wa Shinyanga.
Mwenyekiti wa usalama barabarani Mkoa wa Shinyanga (RSA) Seif Nasolo wakati akipongeza juhudi za serikali kupitia viongozi mbalimbali.
Post a Comment