Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Shirika lisilo la kiserikali la Karibu
Tanzania Organization (KTO) kwa
kushirikiana na Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa TAKUKURU Mkoa wa
Shinyanga na Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Buhangija limewajengea uwezo wa
kupambana na Rushwa ya ngono Chama cha
waendesha baiskeli na waandishi wa habari Mkoa wa Shinyanga.
Mafunzo hayo yametolewa Ijumaa Desemba
16,2022 katika ukumbi wa Mama Samia Shule ya Msingi Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza katika mafunzo hayo
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Karibu Tanzania Organization KTO
Maggid Mjengwa amesema mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo waandishi wa
habari pamoja na waendesha baiskeli hivyo amewataka kuwa mabalozi katika
kuelimisha jamii ili kutokomeza rushwa ya
ngono.
“Ninyi mliopo hapa na zaidi wanahabari mkipata uelewa wa juu ya jambo
hili mtaweza kuisaidia jamii nanyi waendesha baiskeli mnatakiwa
muwe mabalozi wazuri wa kufikisha elimu ya kupambana na rushwa ya ngono katika
jamii”,amesema
Mjengwa.
Kwa upande wake Afisa Uchunguzi
TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Reubeni Chongolo amesema mapambano dhidi ya vitendo
vya rushwa ikiwemo ya rushwa ya ngono yanaweza kukomeshwa endapo jamii
itasimama na kuzingatia maadili mema.
“Sababu pekee ya kuendelea kuwepo kwa rushwa ni mmomonyoko wa maadili
kwahiyo watumishi na watu wote ambao wako kwenye nafasi za kuweza kutoa huduma
wanapokosa kuwa na maadili hupelekea kuomba au kupokea rushwa jambo la msingi
ambalo tunahimiza lazima tusimame kwenye misingi ya uadilifu”.amesema Chongolo
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa
Shinyanga Mwamba Masanja amesisitiza jamii kutofumbia macho vitendo vya rushwa
na kwamba jamii inapaswa kutoa taarifa
sahihi ili TAKUKURU iweze kuchukua hatua.
Hata hivyo Mkuu wa Chuo cha FDC
Buhangija Maria Mkanwa amesema elimu iliyotolewa ni msaada mkubwa katika kuleta
mabadiliko kwenye jamii.
Nao baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wamepata
nafasi ya kuuliza maswali na kujibiwa papo kwa hapo na wataalam kwa lengo la
kuongeza uelewa juu ya rushwa ya ngono.
Baadhi ya washiriki hao wamelipongeza shirika
la KTO kwa kutoa elimu hiyo ya rushwa ya ngono ili iwasaidie katika maisha yao
ya kila siku pamoja na kusaidia jamii.
Mafunzo ya elimu ya rushwa ya ngono
yametolewa siku ya Ijumaa Disemba
16,2022 na kwamba yameratibiwa na Shirika lisilo la kiserikali la Karibu
Tanzania Organization KTO.
Mkurugenzi wa Shirika lisilo la kiserikali la Karibu Tanzania Organization KTO Maggid Mjengwa akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Mkuu wa Chuo cha FDC Buhangija Maria Mkanwa akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Afisa Uchunguzi TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Reubeni Chongolo akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Shinyanga Mwamba Masanja akizungumza kwenye mafunzo hayo
Afisa Habari wa Shirika la
Karibu Tanzania Organization Bi. Symphrose Makungu akizungumza kwenye mafunzo hayo
ya kupinga Rushwa ya Ngono
Post a Comment