" MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 4 ASADIKIKA KUBAKWA FAMILIA YALIOMBA JESHI LA POLISI MKOA WA SHINYANGA KUCHUKUA HATUA KALI

MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 4 ASADIKIKA KUBAKWA FAMILIA YALIOMBA JESHI LA POLISI MKOA WA SHINYANGA KUCHUKUA HATUA KALI

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, limeombwa kufanya uchunguzi wa kina ili kuchukua hatua kali za kisheria kwa mtu aliyehusika na tukio la mtoto wa kike anayesadikika kubakwa mwenye umri wa miaka minne ambaye anasoma  chekechea katika Manispaa ya Shinyanga.

Ombi hilo limetolewa na Familia ya Bwana Paschal Nikolaus mkazi wa kata ya Masekelo Manispaa ya Shinyanga ambapo mlezi wa mtoto huyo Bi. Anna Salehe Mwarabu amesema tukio hilo limetokea Alhamisi Machi 23, Mwaka huu 2023.

Mlezi huyo Bi. Anna Mwarabu ameelezea namna mtoto huyo alivyopotea maada ya kutoka shuleni jioni.

‘Mtoto alitoka shule salama lakini jioni muda wa saa kumi na moja watoto walikuwa wanacheza cheza Mama yao mkubwa aliwaita akakatuma kale kadogo akakaambia hivi kamwite yule mwenzako mje muoge kabla ya baridi kuanza kakaenda wenzie wakasema hayupo Mama yake mkubwa akaenda kumtafuta badaye naye akarudi akasema mtoto nimemkosa akanishikia mtoto na mimi nikaenda kumtafuta nikazunguka sikumuona nikawa naelekezwa nenda sehemu furani kaangalie labda wanaosoma naye hamna sikufanikiwa’

‘Ikabidi nimpigie Baba yao mdogo alikuwa kazini akasema anakuja mi nikaendelea kutafuta badaye nikawaita wale watoto aliokuwa akicheza nao nikawaulizaje hivi nyie mlikuwa mnacheza na mwenzenu mbona kila siku mnacheza naye leo imekuaje haonekani wakati siyo kawaida yake kale kengine kakasemaje yeye si alikubali kwenda na lile libaba nikawauliza libaba gani wakasema lilikuwa limekaa pale kwenye tofali anapokaaga Mama wale watoto wakasema hata sisi lile libaba lilikuwa linatuita yeye akasema haogopi akaenda likaenda kumkubatia mimi sasa nikachanganyikiwa na watu wakawa wengi wakaanza kunisaidia kumtafuta ikabidi nienda kutoa taarifa kwenye mwenyekiti wa mtaa’

‘Baba yake mdogo mara akanipigia simu akaniambia mtoto tumemuona alikuwa nako jamaa tu anatembea huku amekashikilia mkono nimemuuliza akasema amemuokota Relini watu wakawawanamshambulia huyo kijana badaye tukaenda kumweleza Mwenyekiti wa mtaa’

‘Nilipotoka kwa mwenyekiti nikaenda kituoni nikamkuta mtoto tukawa tunamhoji hapo badaye wakasema tukamkague kweli tukaenda kumuangalia ikaonekana mtoto hajachanika ili ameingiliwa kwa sababu tulikuta zile dalili badaye tukapewa PIOF3 baba yake mdogo ndiyo aliendelea naye kumpeleka Hospitali waliambiwa warudi tena asubuhi ya leo ndiyo ameenda tena amebimwa mtoto baadhi ya vipimo ameambiwa atapigiwa simu’

Mama mlezi wa mtoto Bi. Anna Mwarabu pamoja na Baba mzazi wa mtoto huyo Bwana George Nikolaus wameiomba serikali kupitia vyombo vyake kuchunguza kwa kina tukio hilo ili hatua kali za kisheria zichukuliwe kwa mtu aliyehusika.

Mmoja wa majirani katika familia hiyo ambaye hakutaka jina lake kutajwa amesema  matukio mbalimbali ya namna hiyo hutokea katika mtaa huo ambapo wazazi hushindwa kutoa ushirikiano kwenye mamlaka  husika na kwamba kupitia tukio hilo ameiomba serikali kuchukua hatua kali kwa mtu atakayebainika kufanya kitendo hicho.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa mtaa wa Bondeni kata ya Masekelo Juma Idd Maloda amekili kupokea taarifa za tukio hilo ambapo ameeleza kuwa baada ya kufuatilia amebaini kuwa mtu anayedaiwa kuhusika na tukio hilo ni mtu anayeishi mtaa jirani.

“Mtoto yule kwa umri wake inaonekana kuna zezeta alikuja kumlagai akamtorosha ndiyo akaenda kupata zuruba hiyo maana hule mtoto kwa umri wake wa Miaka minne si rahisi kwenda Ibinzamata peke yake inamaana alichukuliwa inamaana alichukuliwa kwa sababu hapo kuna mto sisi huwa tunavuka mto kwanza na huwa tunachukua tahadhari kubwa kwa mtoto kuvuka pale”.

“Tulipopata tukio hilo tuliwasiliana na Polisi kata lakini hata leo mimi nimeenda polisi kwenda kujiridhisha na kweli nimemkuta huyo Bwana aliyekuwa amemchukua mtoto nimemuuliza baadhi ya maswali nikamwuliza unanifahama mimi akasema hapana unaishi mtaa gani akanitajia mtaa jirani basi tunaliomba tu jeshi la Polisi kama kweli huyo mtu anahusika sheria ichukue mkondo wake”.amesema Mwenyekiti wa mtaa Bwana Maloda

Kwa upande wake mganga mfawidhi wa Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Shinyanga Dkt. Luzila John amekili kumpokea mtoto huyo kwa ajili ya kufanya uchunguzi wa vipimo vya awali.

Zimefanyika jitihada mbalimbali za kumpata kaimu kamanda wa jishi la Polisi Mkoa wa Shinyanga lakini hazikufanikiwa mpaka sasa. 

Mtoto wa kike anayesadikika kubakwa mwenye umri wa miaka minne ambaye anasoma  chekechea katika Manispaa ya Shinyanga.

Post a Comment

Previous Post Next Post