" MWENYEKITI WA DOME BWANA CHEUPE AFANYA MKUTANO ROBO MWAKA AHIMIZA WANANCHI KUSHIRIKIANA

MWENYEKITI WA DOME BWANA CHEUPE AFANYA MKUTANO ROBO MWAKA AHIMIZA WANANCHI KUSHIRIKIANA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Rai imetolewa  kwa wananchi wote wa mtaa wa Dome Kata ya Ndembezi Manispaa ya Shinyanga  kuendelea kushirikiana na uongozi wa serikali ya mtaa huo ili kuwabaini wahalifu kwa lengo la kuimarisha usalama.

 Rai hiyo imetolewa na mwenyekiti wa mtaa  wa Dome Bwana Solomon  Najulwa  kwenye Mkutano wake wa hadhara wa robo mwaka ambao umelenga kutoa taarifa za mapato na matumizi ikiwa ni pamoja na kupokea kero mbalimnbali za wananchi.

Bwana Najulwa amesema wananchi wanapaswa kuendelea  kutoa taarifa pindi  wanapobaini viashiria vya  uhalifu na wahalifu ili uongozi huo uweze kushughulikia kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi ambalo lipo kwaajili ya kulinda usalama wa raia na mali zao.

Wakati huo huo Bwana Najulwa amewasisitiza wakazi wa mtaa huo kuzingatia kanuni na taratibu za kuwatambulisha wageni wanaofika kwenye familiza zao katika uongozi wa serikali ili waweze kufahamika jambo ambalo litasaidia kuimarisha ulinzi na usalama.

Katika hatua nyingine baadhi ya wakazi wa mtaa wa Dome wamewaomba wananchi wengine kuwafikisha sehemu husika wageni wanaofika kwenye familia zao ili kuepuka  changamoto zinazoweza kujitokeza.

Katika taarifa yake ameelezea mambo mbalimbali yaliyofanywa na uongozi wa serikali ya mtaa kwa kipindi cha miezi mitatu kuanzia Januari hadi mwezi huu Machi mwaka 2023.

Amesema katika kipindi hicho wamefanikiwa kutambulisha wananchi 115 kupata mkopo katika taasisi za kifedha, waliotambulishwa katika maombi mbalimbali ya kazi 316 na uongozi huo kutatua changamoto 57 za wananchi zinazohusu dawati la Polisi.

Mwenyekiti Najulwa amesema wamewezesha wananchi takribani 275 kupata utambulisho wa Uraia wa NIDA huku akieleza kuwa kwa kipindi hicho uongozi huo umesimamia huduma vizuri kwa walengwa wa TASAF na kusuluhisha migogoro midogomidogo takribani 340 na kusaidia wananchi hao kuendelea kuishi kwa amani.

Amesema kwa upande wa miundombinu ya barabara ujenzi unaendelea vizuri ambapo ameeleza kuwa pamoja na mambo mengine mtaa huo umeendelea kusimamia uwekaji wa vibao vya barabarani kwa ajili ya kutambulisha  eneo husika.

Bwana Nalinga jina maarufu  Cheupe amesema uongozi huo pia umeshirikiana vizuri na wazazi kuhusu elimu ya watoto kuanzia chekechea hadi vyuo vikuu juu ya maadili mema kwa watoto huku akieleza kuwa hakuna changamoto ya usafi wa mazingira na kwamba katika suala la afya uongozi huo umewaandikia barua za msamaha wa matibabu ya bure wazee 35 wenye miaka kuanzia 60.

Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Dome wamewaomba wananchi wengine kuwafikisha sehemu husika wagani wanaofika kwenye familia ili kuepukana na changamoto.


Post a Comment

Previous Post Next Post