Na Elisha Petro, Misalaba Blog
Timu ya mpira wa wavu (Volleyball) kwa upande wa wavulana katoka chuo cha sayansi za Afya Kolandoto kilichopo manispaa ya shinyanga imeishangaza shule ya secondary Don Bosco baada ya ushindi wa jumla ya set 3-0 katika mchezo wa kusisimua uliochezwa katika uwanja wa shule ya secondary don bosco Didia iliyopo halmahsuri ya shinyanga.
Mchezo
huo ni miongoni mwa michezo iliyochezwa
katika bonanza la kuimarisha afya,kudumisha ushirikiano, kuinua pamoja
na kuendeleza vipaji kwa washiriki wote
kwani michezo ni afya na chanzo cha ajira kwa vijana.
Kwa upande wa mpira wa pete Netball wenyeji wa bonanza hilo shule ya sekondari Don Bosco wamekiduwaza chuo cha sayansi za Afya Kolandoto baada ya kuibuka na ushindi wa jumla ya goli 18 – 6.
Kwingineko katika mpira wa kikapu basketball wenyeji shule ya sekondari Don Bosco wamewakaribisha wageni wao kutoka chuo cha sayansi za Afya nkolandoto kwa kichapo cha jumla ya vikapu 79 -70 kwenye mchezo uliochezwa kwa kota nne.Timu ya mpira wa kikapu kutoka chuo cha sayansi za Afya Kolandoto wakitafuta nafasi ya kuwapenya vijana wa shule ya sekondary Don Bosco Didia.
Post a Comment