" HALI YA MITIHANI KIDATO CHA SITA, MKUU WA SHULE BULUBA SEC. AZUNGUMZIA

HALI YA MITIHANI KIDATO CHA SITA, MKUU WA SHULE BULUBA SEC. AZUNGUMZIA

 Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Mitihani ya kidato cha sita katika shule mbalimbali za sekondari Mkoani Shinyanga inaendelea huku wanafunzi wakiahidi kupata matokeo mazuri.

Misalaba Blog imetembelea katika baadhi ya shule ikiwemo Buluba sekondari iliyopo Manispaa ya Shinyanga na kuzungumza na baadhi ya watahiniwa ambapo wamesema tangu kuanza kwa mitihani hiyo Mei 02,Mwaka huu 2023 wameendelea kufanya vizuri kwa mafaniko.

Watahiniwa hao wamesema kutokana na maadalizi mazuri yaliyofanyika kabla ya mitihani hiyo matarajio yao ni kupata ufaulu mzuri.

Akizungumzia mitihani inayoendelea mkuu wa shule ya sekondari Buluba mwalimu Robert Charles amewaomba kuendelea kuzingatia taratibu na kanuni za mitihani ili waweze kuhitimisha zoezi hilo kwa usalama zaidi.

“Mitihani inaendelea vizuri na sisi tuliwaandaa vizuri na wanatarajia kupata matokeo mazuri tu, tutamaliza tarehe 12 Mei 5 mtihani wa mwisho utakuwa ni Physics niendelee tu kuwasihi wazingatia taratibu zote zilizopo na wajiandae tu vizuri kwa mitihani iliyobaki ili wapate matokeo mazuri tayari kwa kujiunga na chuo kikuu”amesema Mwalimu Charles

Mitihani ya kidato cha sita katika shule mbalimbali za sekondari Nchini imeanza Mei 2, 2023 na inatarajiwa kumalizika Mei 12, Mwaka huu 2023.

Post a Comment

Previous Post Next Post