Kamati
tendaji ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kanda ya Serengeti kimemsimamisha
uongozi Mwenyekiti wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Mhe. Emmanuel Ntobi kutokana na
tuhuma za makosa ya kinidhamu.
Akizungumza
Katibu wa kamati ya uenezi wa CHADEMA Kanda ya Serengeti Golden Marcus
amebainisha kuwa kamati tendaji ya Chama hicho imemsimamisha Mheshimiwa Ntobi
kutojihusisha na shughuli zozote za uongozi kwa kipindi cha Mwaka mmoja.
Aidha
Kamati hiyo imemvua uongozi aliyekuwa Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Shinyanga Ndugu
Emmanuel Buyamba ambaye pia anatuhumiwa kwa makossa ya kinidhamu.
“Kikao kilifanyika Tarehe 28, 4,2023 pamoja na Tarehe
29,4,2023 pamoja na mambo mengine ya
kichama yaliyojadiliwa kwenye vikao hivyo, kamati tendaji iliamua kumsimamia
uongozi Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Emmanuel Ntobi na vilevile
kutojihusisha na shughuli zozote za kiuongozi kwa muda wa miezi kumi na mbili
(12) hii yote ni kutokana na makosa ya kinidhamu ndani ya chama”.
“Lakini pia kamanti tendaji ilimvua uongozi aliyekuwa
katibu wa Mkoa wa Shinyanga Ndugu Emmanuel Buyamba naye pia ni kutokana na
makosa ya kinidhamu barua tayari walishapokea”.amesema
katibu wa kanda Marcus
Pamoja
na hatua hiyo Bwana Marcus amebainisha kuwa viongozi hao bado wanaendelea
kutambuliwa kama wanachama halali wa CHADEMA na wana haki ya kukata Rufaa kwa
ngazi za juu kupinga hatua zilizochukuliwa.
Misalaba
Blog imezungumza pia na Mwenyekiti wa CHADEMA aliyesimamishwa uongozi Bwana
Emmanuel Ntobi ambaye amesema hajapata barua rasmi wala nakala ya hukumu ya
adhabu iliyotolewa na chama chake.
“Mpaka sasa hivi tunavyoongea sijapata barua yoyote ya
kusimamishwa wala sijapata nakala ya hukumu ya hiyo adhabu iliyotolewa bahati
mbaya nasikitika sana katibu wa kamati ya uenezi ameongea kwamba amekwisha
nipatia hiyo barua na nakala ya hukumu huu ni mwendelezo tu wa kuona uongozi wa
kanda kunashida kubwa tangu taarifa hiyo itoke siku nne zimepita mimi sijapata
barua rasmi wala nakala ya hukumu bado nasubiria nikishapata barua rasmi na
nakala ya hukumu nitajua na mimi hatua gani nachukua kwahiyo wakileta hivo vitu
nitafanya maamuzi na mimi”.amesema Mhe. Ntobi
Hata
hivyo hazikufanikiwa juhudi za kumpata aliyekuwa katibu wa chama hicho Mkoa wa
Shinyanga Bwana Emmanuel Buyamba ambaye licha ya kupigiwa simu lakini iliita
bila kupokelewa.

Post a Comment