" BODABODA MBALONI KWA MAUAJI YA MTOTO

BODABODA MBALONI KWA MAUAJI YA MTOTO


Na Belnardo Costantine, MisalabaMedia

 Jeshi la Polisi Mkoani Iringa linamshikilia Joseph  Muhulila (28) Mwendesha Bodaboda  na Mkazi wa Mtaa wa Lukosi kata ya Mkwawa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Kwa tuhuma za mauaji Mtoto wake aliyejulikana kwa Timotheo Joseph Muhulila mwenye umri wa miaka 6 Kwa  kumchinja  na kutenganisha viungo  vyake Kisha kutupa mabaki ya mwili kwenye shimo la Choo.

 Mwenyekiti wa mtaa wa Lukosi Kenedi mahona amesema ni wiki tatu zimepita tangu mzazi huyo alipotoa taarifa za kupotelewa  amtoto wake,
baada uya upelelezi wa jeshi la polisi amekiri kuhusika kwenye mauaji hayo.

Hata hivyo Mkaguzi msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji MelkSedeck Banzi amesema wametoa baadhi ya vipande vya nyama ambapo bado haijathibitishwa Moja Kwa Moja  kama ni vipande vya Binadamu.
sambamba  na hilo  Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Iringa SACP Allan Bukumbi akithibitisha kutokea Kwa tukio hilo.


Post a Comment

Previous Post Next Post