

Na Mapuli Kitina
Misalaba
Baraza Maalum la
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga limepokea, kujadili na kupitisha
Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru katika kikao
kilichofanyika leo Juni 19, 2025, katika ukumbi wa makao makuu ya Halmashauri hiyo.
Akizungumza kwenye
mkutano huo, Wakili wa Serikali wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Salehe
Hassan amesema marekebisho hayo yanalenga kuboresha ukusanyaji wa mapato ya
ndani na kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi kwa kuzingatia sheria na taratibu
zilizopo.
Kwa upande wake
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Ngassa Mboje
amewapongeza madiwani kwa kushiriki kikamilifu katika kupitia na kujadili
rasimu hiyo, akisema hatua hiyo ni ishara ya uwajibikaji katika kusimamia
rasilimali za umma.
Mkurugenzi wa
Halmashauri hiyo, Dkt. Kalekwa Kasanga amesema Halmashauri itaendelea
kushirikiana na wadau wote kuhakikisha utekelezaji wa sheria hizo unaleta
matokeo chanya kwa maendeleo ya wananchi.
Mkuu wa Wilaya ya
Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro amepongeza hatua hiyo ya baraza akisema ni
sehemu ya mageuzi ya kimfumo ya kusimamia mapato na kutoa huduma bora, huku
akiwasihi madiwani kuendelea kuwa mabalozi wa elimu ya mapato katika kata zao.
Naye Mwenyekiti wa
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Vijijini, Mhe. Edward Ngelela
amesema chama kinatambua umuhimu wa marekebisho hayo na kitaendelea
kushirikiana na serikali kuhakikisha wananchi wanaelimishwa kuhusu umuhimu wa
kulipa ushuru na ada kwa maendeleo ya maeneo yao.
Rasimu hiyo ni nyenzo
muhimu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga katika kuhakikisha kuwa mfumo wa
ukusanyaji wa mapato unakwenda sambamba na mahitaji halisi ya sasa ya
maendeleo.
Kupitia marekebisho haya, Halmashauri inalenga: Kuboresha
vyanzo vya mapato ya ndani, ili iweze kugharamia miradi ya maendeleo na huduma
muhimu kama elimu, afya, barabara na maji.
Lakini pia kuweka uwiano wa haki kati ya wananchi na
serikali, kwa kuhakikisha kuwa ada na ushuru unatozwa kwa uwazi na kwa viwango
vinavyokubalika, Kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato, kwa kuweka misingi ya
kisheria inayoeleweka vizuri na inayotekelezeka.
Pamoja na kuhamasisha ulipaji wa ushuru kwa hiari kwa
kuwa na sheria ndogo zinazoeleweka na zinazozingatia mazingira ya wananchi.
Kwa kifupi, rasimu hiyo ni msingi wa kujenga Halmashauri yenye uwezo wa kifedha na inayowajibika kwa wananchi wake.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Ngassa Mboje, akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani ambao leo Juni 19, 2025 wamepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga,
Mhe. Ngassa Mboje, akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani ambao leo Juni
19, 2025 wamepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo
za Ada na Ushuru.

Wakili wa Serikali wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Salehe Hassan akisoma Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru katika kikao hicho leo Juni 19, 2025.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Dkt. Kalekwa Kasanga akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani ambalo leo Juni 19, 2025 limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.
Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga likiendelea ambapo leo limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambalo leo Juni 19, 2025 limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambalo leo Juni 19, 2025 limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.

Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya
ya Shinyanga likiendelea ambapo leo limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya
Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.
Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya
ya Shinyanga likiendelea ambapo leo limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya
Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro akizungumza
kwenye Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambalo
leo Juni 19, 2025 limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya
Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.




Post a Comment