" HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA YAPITISHA RASIMU YA MAREKEBISHO YA SHERIA NDOGO ZA ADA NA USHURU

HALMASHAURI YA WILAYA YA SHINYANGA YAPITISHA RASIMU YA MAREKEBISHO YA SHERIA NDOGO ZA ADA NA USHURU

Na Mapuli Kitina Misalaba

Baraza Maalum la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga limepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru katika kikao kilichofanyika leo Juni 19, 2025, katika ukumbi wa makao makuu ya Halmashauri hiyo.

Akizungumza kwenye mkutano huo, Wakili wa Serikali wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Salehe Hassan amesema marekebisho hayo yanalenga kuboresha ukusanyaji wa mapato ya ndani na kutoa huduma bora zaidi kwa wananchi kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Ngassa Mboje amewapongeza madiwani kwa kushiriki kikamilifu katika kupitia na kujadili rasimu hiyo, akisema hatua hiyo ni ishara ya uwajibikaji katika kusimamia rasilimali za umma.

Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Dkt. Kalekwa Kasanga amesema Halmashauri itaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha utekelezaji wa sheria hizo unaleta matokeo chanya kwa maendeleo ya wananchi.

Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Wakili Julius Mtatiro amepongeza hatua hiyo ya baraza akisema ni sehemu ya mageuzi ya kimfumo ya kusimamia mapato na kutoa huduma bora, huku akiwasihi madiwani kuendelea kuwa mabalozi wa elimu ya mapato katika kata zao.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Shinyanga Vijijini, Mhe. Edward Ngelela amesema chama kinatambua umuhimu wa marekebisho hayo na kitaendelea kushirikiana na serikali kuhakikisha wananchi wanaelimishwa kuhusu umuhimu wa kulipa ushuru na ada kwa maendeleo ya maeneo yao.

Rasimu hiyo ni nyenzo muhimu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga katika kuhakikisha kuwa mfumo wa ukusanyaji wa mapato unakwenda sambamba na mahitaji halisi ya sasa ya maendeleo.

Kupitia marekebisho haya, Halmashauri inalenga: Kuboresha vyanzo vya mapato ya ndani, ili iweze kugharamia miradi ya maendeleo na huduma muhimu kama elimu, afya, barabara na maji.

Lakini pia kuweka uwiano wa haki kati ya wananchi na serikali, kwa kuhakikisha kuwa ada na ushuru unatozwa kwa uwazi na kwa viwango vinavyokubalika, Kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato, kwa kuweka misingi ya kisheria inayoeleweka vizuri na inayotekelezeka.

Pamoja na kuhamasisha ulipaji wa ushuru kwa hiari kwa kuwa na sheria ndogo zinazoeleweka na zinazozingatia mazingira ya wananchi.

Kwa kifupi, rasimu hiyo ni msingi wa kujenga Halmashauri yenye uwezo wa kifedha na inayowajibika kwa wananchi wake. 

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Ngassa Mboje, akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani ambao leo Juni 19, 2025 wamepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Mhe. Ngassa Mboje, akizungumza kwenye Baraza Maalum la Madiwani ambao leo Juni 19, 2025 wamepokea, kujadili na kupitisha Rasimu ya Marekebisho ya Sheria Ndogo za Ada na Ushuru.





 

Post a Comment

Previous Post Next Post