Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Yanga Sc ametoa ufafanuzi kuhusu mkataba wa kiungo Stephanie Aziz Ki na klabu ya Wydad Casablanca na kueleza kuwa makubaliano yao ilikuwa ni kuwatumikia Wydad kwa mkataba wa miezi mitatu.
Kamwe amebainisha kwamba mkataba huo una vipengele viwili ambapo ikiwa miamba hiyo ya Morocco itaridhishwa na kiwango chake basi watamuongezea mkataba wa miaka miwili na ikiwa vinginevyo basi atarejea Jangwani na atakuwepo kwenye mchezo wa Ngao ya Jami..
“Kwa mujibu wa makubaliano ilikuwa hadi kufikia Julai 10 Wydad wawe wameshawasiliana na Yanga Sc. Kama Wydad watakuwa wanaongeza maana yake wamalizie kiasi ambacho tulikubaliana ila kama watasema arudi sawa arudi aje awashone maana bado amebaki na mwaka mmoja.”——amesema Kamwe.
Katika hatua nyingine, Kamwe ameweka wazi kuwa tayari kocha mpya ameshatua klabuni hapo na kwa sasa anapitia ‘mafaili’ ya watangulizi wake kabla ya kutambulishwa rasmi na kuanza mchakato wa usajili.
Kamwe amebainisha kwamba mkataba huo una vipengele viwili ambapo ikiwa miamba hiyo ya Morocco itaridhishwa na kiwango chake basi watamuongezea mkataba wa miaka miwili na ikiwa vinginevyo basi atarejea Jangwani na atakuwepo kwenye mchezo wa Ngao ya Jami..
“Kwa mujibu wa makubaliano ilikuwa hadi kufikia Julai 10 Wydad wawe wameshawasiliana na Yanga Sc. Kama Wydad watakuwa wanaongeza maana yake wamalizie kiasi ambacho tulikubaliana ila kama watasema arudi sawa arudi aje awashone maana bado amebaki na mwaka mmoja.”——amesema Kamwe.
Katika hatua nyingine, Kamwe ameweka wazi kuwa tayari kocha mpya ameshatua klabuni hapo na kwa sasa anapitia ‘mafaili’ ya watangulizi wake kabla ya kutambulishwa rasmi na kuanza mchakato wa usajili.
Post a Comment