" NGOS ZINAZOFANYA KAZI KWENYE SEKTA YA UVUVI ZAKUTANA

NGOS ZINAZOFANYA KAZI KWENYE SEKTA YA UVUVI ZAKUTANA

Edwin Soko (TMFD)
Tanga

Mashirika yasiyo ya kiserikali yanayofanya kazi kwenye sekta ya uvuvi yamekutana Jijini Tanga kuweka mikakati ya kufanya kazi Kwa  kushirikiana baiana ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi na mashirika hayo.

Mkutano huo umeratibiwa  na Wizara ya mifugo na uvuvi Kwa kukutanisha mashirika ya yasiyo ya kiserikali mbalimbali.

Mkurugenzi wa Uvuvi Profesa.  Prof. Mohammed Sheikh alisema  kuwa, kikao hicho ni muhimu sana Kwa kuwa kinatoa fursa kwa Wizara kusikiliza wadau wanasema nini juu ya kazi zinazofanya na Wizara na nini changamoto za kisekta na namna gani ya kuzitatua.

Profesa Sheikh pia  amewashukuru wawakilishe wote wa mashirika na kupata nafasi ya kuwapitisha kwenye vipaumbele vinne vya Wizara ya mifugo na uvuvi Tanzania.

Naye Mratibu wa mashirika ya yasiyo ya kiserikali toka dawati la uvuvi  Tumaini Chambua alipata  nafasi ya kuwapitisha washiriki kwenye mwongozo wa mashirikiano  baina ya Wizara (sekta ya uvuvi)na mashirika yasiyo ya kiserikali.

Mkutano huo ni wa siku mbili na umeshirikisha mashirika yasiyo na kiserikali ya ndani ya Nchi, kimataifa na Wizara ya mifugo na uvuvi.

Mkurugenzi wa Uvuvi Prof.Mohammed Sheikh akifungua kikao Kati ya Wizara ya mifugo na Uvuvi na Asasi zisizo na kiserikali


Post a Comment

Previous Post Next Post