" MGODI WA NYANDOLWA: WATU 11 WATOLEWA, NANE WAFARIKI DUNIA

MGODI WA NYANDOLWA: WATU 11 WATOLEWA, NANE WAFARIKI DUNIA

Na Mapuli Kitina Misalaba

Zoezi la uokoaji katika machimbo ya Nyandolwa wilayani Shinyanga linaendelea, ambapo hadi sasa watu 11 wametolewa kati ya wachimbaji 25 waliofunikwa na mgodi Agosti 11, mwaka huu 2025.

Kati ya waliotolewa, watatu wameokolewa wakiwa hai na nane wakiwa wamefariki dunia, huku juhudi za kuwapata wachimbaji wengine 14 zikiendelea kwa kutumia mashine za utambuzi wa ardhini ili kubaini walipo.

Mnamo Agosti 16, 2025 Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga, Julius Mtatiro, aliagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga, Dkt. Kalekwa Kasanga, kuweka ofisi ya muda ya mtendaji wa kijiji katika eneo la tukio kwa ajili ya kusajili wageni na kuratibu huduma zinazotolewa na serikali.

Aidha, Agosti 18, 2025 Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mboni Mhita, alielekeza familia ambazo ndugu zao bado hawajaokolewa kuteua wawakilishi wachache watakaobaki eneo la tukio ili kurahisisha utaratibu wa serikali kuwapatia mahitaji muhimu.

Leo Agosti 23, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi, akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa maagizo kwa viongozi wa serikali waliopo eneo la ajali kushiriki kikamilifu kwenye taratibu za mazishi ya waathirika na kuwasilisha rambirambi za Rais katika familia husika.

“Rais Samia kaniagiza kuwafikishia salamu za pole na rambirambi, pia kanituma kuleta maagizo kwa viongozi waliopo eneo hili kuhakikisha wanahudhuria misiba yote ya watu waliopoteza maisha katika ajali hii na kuwakilisha rambirambi alizotoa katika familia hizo,” amesema Lukuvi.     

GUSA LINK HAPA CHINI👇


🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA



Post a Comment

Previous Post Next Post