" MGOMBEA UBUNGE AZZA HILLAL AWAOMBA WANANCHI WA ITWANGI KURA ZA NDIYO KWAKE, DKT. SAMIA NA MGOMBEA MWENZA DKT. NCHIMBI

MGOMBEA UBUNGE AZZA HILLAL AWAOMBA WANANCHI WA ITWANGI KURA ZA NDIYO KWAKE, DKT. SAMIA NA MGOMBEA MWENZA DKT. NCHIMBI


Na Mapuli Kitina Misalaba


Katika kampeni zinazoendelea kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, Mgombea Ubunge wa Jimbo Jipya la Itwangi lililopo Mkoani Shinyanga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Azza Hillal Hamad, amejitokeza mbele ya wananchi na kuwaomba kumpa kura za ndiyo ili aweze kuwatumikia kwa uadilifu na kuleta maendeleo ya haraka katika jimbo hilo jipya.

Akizungumza na Misalaba Media wakati wa mkutano mkubwa wa kampeni uliofanyika Wilaya ya Kishapu na mjini Shinyanga kwa lengo la kunadi sera na Ilani ya CCM, Azal Hilal amewashukuru wananchi wa Itwangi kwa mapokezi makubwa na kuonyesha mshikamano wao na chama hicho, akiwahimiza kuendeleza mshikamano huo kwa kujitokeza kwa wingi siku ya uchaguzi.

“Naomba wananchi wenzangu wa Jimbo la Itwangi mnipe kura za ndiyo ili niwe mwakilishi wenu bungeni. Pia naomba tumuunge mkono kwa kura za ndiyo Mama yetu Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mgombea Mwenza Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ili tuhakikishe maendeleo yanaendelea kwa kasi na nchi yetu inasonga mbele kwa mshikamano na amani,” amesema Azza.

Azza Hillal amesisitiza kuwa ushindi wa pamoja kwa CCM kuanzia nafasi ya Rais, Wabunge na Madiwani ni muhimu kwa utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya 2025–2030 bila vikwazo, na kwamba wananchi wa Itwangi watapata nafasi ya kushuhudia miradi mikubwa ya kimaendeleo ikitekelezwa kwa kasi katika eneo lao.

Aidha, ameahidi kushirikiana kwa karibu na wananchi mara baada ya kuchaguliwa, akiahidi kutetea maslahi ya wananchi wa Itwangi kwa kuzingatia mahitaji ya sekta muhimu kama elimu, afya, barabara, maji safi na salama, pamoja na fursa za ajira kwa vijana.

Mgombea Ubunge wa Jimbo Jipya la Itwangi lililopo Mkoani Shinyanga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Azza Hillal Hamad, akizungumza.Mgombea Ubunge wa Jimbo Jipya la Itwangi lililopo Mkoani Shinyanga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Azza Hillal Hamad, akizungumza.

 

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post