" RASMI: ZUNGU SPIKA MPYA WA BUNGE LA TANZANIA

RASMI: ZUNGU SPIKA MPYA WA BUNGE LA TANZANIA





‎ ‎Mhe. Mussa Azzan Zungu Spika mpya wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungnao wa Tanzania. ‎

‎Zungu amechaguliwa kushika nafasi hiyo baada ya aliyekuwa Spika wa bunge hilo, Dkt. Tulia ackson, kutangaza kujiondoa katika mbio za kugombea Uspika wa bunge. ‎

‎Zungu ambaye ni mbunge wa Jimbo la Ilala Jijini Dar es salaam kupitia Chama cha Mapinduzi CCM alikuwa ni miongoni wa wagombea 6 waliojitokeza kugombea nafasi hiyo,ambapo yeye pekee alikuwa anatoka bungeni na wagombea 5 wametoka nje ya bunge wakiwakilisha vyama vingine vya siasa. ‎ ‎

Zungu amechaguliwa kwa kura 378 kati ya 383 zilizopigwa kutoka kwa wabunge wa bunge la Tanzania, huku kura 3 zikiharibika.

Post a Comment

Previous Post Next Post