" TUME YA UCHUNGUZI NDIYO JUKWAA LA KISHERIA

TUME YA UCHUNGUZI NDIYO JUKWAA LA KISHERIA

Serikali ya Awamu ya Sita imesisitiza kuwa Watanzania hawana sababu yoyote ya kuitikia miito ya vurugu na maandamano, kwani tayari Tume ya Uchunguzi iliyoundwa na Rais Samia Suluhu Hassan ndiyo jukwaa rasmi na la kisheria la kushughulikia kiini cha vurugu za Oktoba 29, 2025. Huku Serikali ikisisitiza kazi ya Tume, viongozi wa dini wameonya kuwa matukio ya vurugu za awali yatoe funzo la kutosha kwa taifa.

Serikali imeeleza wazi kuwa Tume hiyo, inayoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu Mohamed Chande Othmani, imesheheni mamlaka ya kuchunguza mambo mawili makuu yenye utata:Chanzo cha Fedha: Kutafuta kwa kina fedha walizolipwa vijana waandamanaji walioshiriki kwenye vurugu na ushiriki wa Taasisi Zisizo za Serikali (NGO), za ndani na za nje, zilizochangia katika kufadhili vurugu hizo.

Madhumuni makuu ya Rais Samia ni Tume "kutafuta majibu ya kitaalamu kwa maswali haya ili kulinda vijana na rasilimali za nchi."

Kwa kuwa Serikali imechukua jukumu hili la msingi, wananchi wote, hususan vijana, wanatakiwa kuepuka kabisa miito yoyote ya maandamano au vurugu inayoenezwa mitandaoni, kwani hoja za msingi zenye utata sasa ziko chini ya uchunguzi wa kitaifa.

Kauli ya Serikali imeungwa mkono na viongozi wa dini, ambao wamewataka waumini wote kuepuka vitendo vinavyoweza kusababisha machafuko.

Bw. Sherally Hussein Sherally, Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Msikiti wa Al Jumaa jijini Mwanza, amesema matukio ya Oktoba 29 yametoa funzo muhimu kwa taifa, akionya kuwa vurugu hizo zilitokana na baadhi ya watu kudhania kuwa ni masuala madogo, ilihali matokeo yake yalikuwa makubwa.

“Sisi kama Waislamu tunapinga vikali hatua zozote au maneno yoyote au taasisi yoyote au chama chochote ambacho kina malengo ya kuleta vurugu katika nchi hii,” alisema Bw. Sherally akisisitiza, “Vurugu zilizotokea Oktoba 29 zimetupa funzo, na kuna wakati tulidhania ni masihara lakini hayakuwa masihara tumeona matokeo yake.”

Bw. Sherally pia alitoa onyo kali kuhusu taarifa zinazodai kuwepo kwa makundi yanayopanga kuandamana Desemba 9, akieleza kuwa siku hiyo ni maalumu kwa maadhimisho ya Uhuru wa Tanganyika, hivyo haipaswi kuchanganywa na masuala ya vurugu.

“Kwahiyo Desemba 9 kujitokeza kwa kile wanachokitaka kufikisha ujumbe wanaoutaka sio siku yake, hiyo ni siku ya sherehe, tunataka kusherekea uhuru wa Tanganyika, tusiingiziwe kitu mbadala wa sherehe tulizokuwa tumeandaa,” alisema Bw. Sherally.

Wito wa Serikali na viongozi wa dini unasisitiza kuwa suluhisho la changamoto za kisiasa sasa lipo chini ya uchunguzi wa Tume, na ni wajibu wa kila Mtanzania kutoa nafasi kwa Tume hiyo ya kisheria kufanya kazi yake badala ya kuanzisha vurugu mpya.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254



Post a Comment

Previous Post Next Post