Kikundi cha sanaa cha SHY TALENT FILMS leo Ijumaa Januari 16, 2026 kimeendelea
na mazoezi mbalimbali ya utayari, ikiwa ni maandalizi ya kutengeneza filamu au
tamthilia mpya zitakazolenga kuelimisha jamii kupitia sanaa.
Mazoezi hayo yamefanyika
katika mazingira ya nidhamu na ushirikiano mkubwa miongoni mwa wanakikundi,
yakilenga kuimarisha uigizaji, mawasiliano ya jukwaani pamoja na uelewa wa
ujumbe unaotarajiwa kufikishwa kwa jamii.
Mazoezi hayo yamehudhuria
na Mtendaji wa Mtaa wa Miti Mirefu, Angelight Emmanuel
Mwanri, ambaye baada
ya kushuhudia mwenendo wa mazoezi amewapongeza vijana hao kwa juhudi na ari
waliyonayo, huku akiwatia moyo kuendelea kujifunza, kufanya kazi kwa bidii na
kutokukata tamaa katika safari ya sanaa.
Kwa upande wa uongozi wa
kikundi, mazoezi ya leo yameshirikiwa na Katibu wa SHY TALENT FILMS
Daniel Sibu, Mkurugenzi wa Misalaba Media Mapuli Misalaba, Mwenyekiti
wa SHY TALENT FILMS Daniel Elimboto, pamoja na walimu wa kikundi hicho akiwemo John Jackson, ambao wameendelea kutoa miongozo na
maelekezo kwa wanakikundi ili kuhakikisha kazi zinazotarajiwa zitakuwa na ubora
na maudhui yenye tija kwa jamii.
SHY TALENT FILMS
inaendelea kujipambanua kama jukwaa la kukuza vipaji vya vijana na kuitumia
sanaa kama nyenzo ya kuelimisha, kuhamasisha na kuijenga jamii ya Manispaa ya
Shinyanga na Tanzania kwa ujumla.
Mazoezi hayo yanaendelea
kesho Jumamosi katika ofisi ya Misalaba Media ilizopo Mjini Shinyanga karibu na Stand ya Zamani, kuanzia saa
kumi kamili jioni.
Mtendaji wa Mtaa wa Miti Mirefu, Angelight Emmanuel Mwanri, akipongeza kwa mazoezi hayo.
Mazoezi ya kikundi cha SHY TALENT FILMS yakiendelea katika ofisi ya Misalaba Media, Mjini Shinyanga, ikiwa ni maandalizi ya kuendeleza vipaji mbalimbali ikiwemo filamu na tamthilia.
Mazoezi ya kikundi cha SHY TALENT FILMS yakiendelea katika ofisi ya Misalaba Media, Mjini Shinyanga, ikiwa ni maandalizi ya kuendeleza vipaji mbalimbali ikiwemo filamu na tamthilia.🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254

















Post a Comment