Mpanda. Kamati Ndogo ya Ufuatiliaji wa Shule ya
Sekondari na Ufundi Milala imefanya kikao cha dharura tarehe Aprili 1, 2026,
kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo ya shule hiyo, hususan upangaji na
upimaji wa eneo la shule kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya kimkakati.
Kikao hicho kilifunguliwa na
Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Mpanda, Ndg. Jimotoli Jilala Maduka,
ambaye aliwakaribisha wajumbe na kuwataka kuwa watulivu wakati wa kikao pamoja
na kuchangia mada zilizowasilishwa kwa lengo la kufanikisha maamuzi yenye tija.
Katika hatua ya utambulisho, Katibu huyo
aliwatambulisha wajumbe mbalimbali wa kamati ndogo ya ufuatiliaji ili kujenga
uelewano na mshikamano katika utekelezaji wa majukumu yao.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Ndg. Jimotoli
Jilala Maduka aliwasilisha agenda ya upangaji na upimaji wa eneo la Shule ya
Sekondari na Ufundi Milala, akieleza umuhimu wa zoezi hilo katika kuweka msingi
imara wa maendeleo ya shule hiyo. Wajumbe wa kamati hiyo waliunga mkono agenda
hiyo na kusisitiza kuwa upangaji na upimaji wa eneo la shule ni hatua muhimu
itakayowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi.
Aidha, kikao hicho kilijadili suala la upatikanaji wa
fedha kwa ajili ya kugharamia zoezi la upangaji na upimaji, ambapo wajumbe
walikubaliana kupambana kwa pamoja kuhakikisha fedha zinapatikana. Kamati hiyo
ilitoa wito kwa wadau mbalimbali na wananchi wenye mapenzi mema na maendeleo ya
elimu kujitokeza kuchangia ili kufanikisha zoezi hilo muhimu kwa mustakabali wa
shule hiyo.
Mwenyekiti aliwashukuru wajumbe kwa mahudhurio yao, michango, mawazo na mapendekezo yao yaliyolenga kuboresha ufuatiliaji wa maendeleo ya Shule ya Sekondari na Ufundi Milala pamoja na kuimarisha shughuli za Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Mpanda.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda na Mwenyekiti wa kikao hicho, akifungua kikao cha dharura.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, akiwasomea wajumbe agenda katika kikao cha ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda na mjumbe wa Kamati Ndogo ya Ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala, akichangia agenda katika kikao hicho huku akiwahimiza wajumbe kuwa na umoja na mshikamano ili kuhakikisha mradi wa shule unapangwa na kupimwa, hatua itakayowezesha kupatikana kwa hati miliki ya shule hiyo. Aidha, alisisitiza kuwa kwa nia na ushirikiano, malengo hayo yanaweza kufikiwa.
Ndg. Rashid Masoud Nsekela, Mhandisi wa Maji kutoka Bonde la Ziwa Rukwa, akitoa maelekezo katika kikao cha ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala kuhusu masuala ya bonde la maji, hususan namna sahihi ya upimaji wa eneo la shule.
Ndg. Hawa, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Kata ya Misunkumilo na mjumbe wa Kamati Ndogo ya Ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala, akichangia agenda katika kikao hicho kwa lengo la kupanua wigo wa maendeleo ya shule hiyo na kuhamasisha wadau wenye mapenzi mema kujitokeza kuunga mkono juhudi hizo, huku akisisitiza umuhimu wa shule hiyo kama eneo la kimkakati kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii.
Ndg. Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Kata ya Nsemulwa na mjumbe wa Kamati Ndogo ya Ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala akichangia agenda mbalimbali katika kikao hicho.
Ndg. Jimotoli Jilala Maduka, Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Mpanda, akiendelea kuchangia mawazo mbalimbali kuhusu agenda husika katika kikao cha ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala.
Ndg. Agnes Raphael, Katibu wa Malezi Kata ya Mpanda Hotel na mjumbe wa Kamati Ndogo ya Ufuatiliaji wa Shule ya Sekondari na Ufundi Milala, akichangia agenda katika kikao hicho akisisitiza umuhimu wa upangaji na upimaji wa shule hiyo ili kuimarisha upatikanaji wa elimu na kuvutia wawekezaji katika Manispaa ya Mpanda, Mkoa wa Katavi.SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




Post a Comment