Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Judith Kapinga (Mb) , amesema Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yameonyesha mafanikio makubwa ya sekta ya viwanda na biashara pamoja na fursa zinazotolewa na Serikali kwa vijana na wanawake.
Waziri Kapinga amesema hayo akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Waziri Salum, alipotembelea maonesho hayo julai 01, 2026 yanayoshirikisha waoneshaji 3,722 kutoka nchi 23 ambayo yatafunguliwa rasmi Julai 3 na Rais wa Msumbiji, Mhe. Daniel Francisco Chapo, akiwa ameambatana na Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Aidha, amewataka Watanzania kutembelea maonesho hayo ili kujifunza kuhusu biashara, viwanda na fursa za kuongeza thamani ya mazao.
Amesema bidhaa nyingi zinazozalishwa na wanawake na vijana zinaonesha matokeo ya uwekezaji wa Serikali kupitia mikopo na programu za uwezeshaji.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254
Post a Comment