Mwenyekiti
wa Machifu Tanzania na Mtemi wa Himaya ya Jigoku, Chifu Antonia Sangalali,
amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kujiandaa mapema kukabiliana na athari
zinazoweza kusababishwa na mvua zinazohusishwa na hali ya El Niño.
Chifu
Sangalali ametoa wito huo wakati wa Tamasha la 19 la Himaya ya Jigoku, Masela,
Wilaya ya Maswa mkoani Simiyu, akiwataka wananchi kutunza chakula na kuchukua
tahadhari dhidi ya uwezekano wa kutokea kwa mafuriko katika maeneo mbalimbali.
Amesema
wananchi wanaoishi katika maeneo hatarishi wanapaswa kuwa makini na kuondoka
mapema endapo wataona hali ya mvua kubwa inayoweza kuhatarisha usalama wao.
“Kuna
mvua za El Niño zinazoelezwa kutokea mwaka huu. Tutakuwa na mafuriko, niwaombe
tunzeni chakula, mjiangalie sana, chukueni tahadhari mapema. Mkiona mvua za El
Niño, mtoke sehemu hatarishi,” amesema Chifu Sangalali.
Taarifa ya
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) iliyotolewa Agosti 18, 2026, inaeleza
kuwa msimu wa mvua za Vuli wa Oktoba hadi Desemba 2026 unatarajiwa kuathiriwa
kwa kiwango kikubwa na hali ya El Niño yenye nguvu kubwa.
Chifu
Sangalali amesisitiza kuwa maandalizi ya mapema ni muhimu ili kulinda maisha ya
wananchi, chakula na mali zao dhidi ya athari zinazoweza kujitokeza kutokana na
mvua hizo.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254




Post a Comment