" PANGANI NA NEEMA YA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA KUCHAKATA MADINI YA MCHANGA WA BAHARINI

PANGANI NA NEEMA YA UWEKEZAJI WA KIWANDA CHA KUCHAKATA MADINI YA MCHANGA WA BAHARINI

 


NA: DK. REUBENI LUMBAGALA 

Sekta vya viwanda ni injini ya maendeleo ya uchumi kutokana na kufungamanishwa kwake na fursa mbalimbali za maendeleo.

Katika jitihada za kuinua maendeleo ya watu na ya uchumi, viwanda havipaswi kuachwa nyuma kwani vina mchango mkubwa katika kufanikisha azma hiyo.

Nchi nyingi zilizoendelea zilifanikiwa katika mipango ya maendeleo kutokana na kuipa msukumo mkubwa sekta ya viwanda

Katika mikakati ya kujenga na kuinua uchumi wa Tanzania, serikali imeweka mazingira bora na wezeshi kwa ajili ya uwekezaji za viwanda huku seta binafsi ikipewa nafasi kubwa ya kuwekeza katika viwanda.

Mkoa wa Tanga umekuwa na historia kubwa nchini kwa kuwa na maendeleo makubwa ya viwanda, lakini katika miaka ya nyuma viwanda vingi vilikufa.

Juhudi za makusudi zimekuwa zikifanywa na serikali kwa kuhakikisha viwanda vilivyokufa vinafufuliwa huku ujenzi wa viwanda vipya ukifanyika kwa kuishirikisha kikamilifu sekta binafsi.

Sasa ni dhahiri maamuzi ya kuurejesha mkoa wa Tanga katika hadhi yake ya maendeleo ya viwanda yanaendelea kutekelezwa kwa vitendo na matunda yake yameanza kuonekana kwa macho ya damu na nyama.

Katika wilaya ya Pangani mkoani Tanga, neema ya maendeleo imeshuka. Hii ni baada ya kampuni ya Shenghe Resource ya nchini China kuamua kuwekeza kiwanda kikubwa cha kuchakata madini ya mchanga mzito wa baharini (Heavy Mineral Sands).

Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, akiwa ziarani China, amehakikishiwa mradi huo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Shenghe, Xie Bing.

Kimsingi, utekelezaji wa mradi huo unafungua na kuongeza fursa za ajira, jambo litakalochochea ustawi wa maisha ya wananchi.


Aidha, kupitia mradi huo, mapato ya serikali yataongezeka kupitia ulipajikodi serikalini, ambapo kodi hizo zitasaidia uboreshaji wa sekta nyingine kama elimu, afya, maji, kilimo, uvuvi na miundombinu.

Vilevile, kuongezeka kwa fursa za biashara. Sekta binafsi itanufaika kwa uanzishwaji wa shughuli za biashara kama migahawa, hoteli na maduka ya bidhaa mbalimbali.

Ni kwamba, ujenzi wa kiwanda hicho cha kuchakata mchanga wa bahari barani Afrika kinachojengwa katika ardhi ya Pangani itachangia kuleta mageuzi makubwa ya kiuchumi Pangani na Tanzania kwa ujumla. 

Pamoja na hayo, Pangani pia kuna mradi mkubwa wa mashamba ya miwa pamoja na ujenzi wa kiwanda cha sukari kinachogharimu zaidi ya shingi bilioni 900 za Kitanzania. 

Kwa hakika, hadhi ya Tanga ya viwanda na maendeleo ya viwanda nchini inazidi kukua kwa kasi zaidi kutokana na utashi mkubwa wa kisiasa wa serikali ya Awamu ya Sita, chini ya uongozi wa Rais Dk. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya viwanda na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla.

PROFESSOR MGOKO SERIES (EP 1)



Post a Comment

Previous Post Next Post