" TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA YASISITIZA MATUMIZI YA MFUMO WA TEHAMA KAMA DARAJA LA UTOAJI HAKI NCHINI

TUME YA UTUMISHI WA MAHAKAMA YASISITIZA MATUMIZI YA MFUMO WA TEHAMA KAMA DARAJA LA UTOAJI HAKI NCHINI

Na Moshi Ndugulile, Shinyanga

Jaji kiongozi wa Tanzania na kamishna wa tume ya utumishi wa Mahakama Nchini  Mheshimiwa MUSTAPHER SIYANI amewataka wadau wa Mahakama wakiwemo watendaji hasa   mawakili kujiandaa katika matumizi ya mfumo wa tehama kama daraja la utoaji haki Nchini

Akitoa mada kuhusu ushiriki wa wadau katika jukumu la utoaji wa haki kwenye Mkutano kati ya tume ya utumishi wa Mahakama pamoja na wadau wa Mahakama wa Mkoa wa Shinyanga,ikiwa ni sehemu ya ziara ya tume ya utumishi wa Mahakama katika Mikoa ya Shinyanga na Simiyu, alisema dhamira ya  Mahakama ya Tanzania ni kuhakikisha kwamba inapunguza na hatimaye kuachana na matumizi ya analojia katika shughuli zake,kuongeza uwazi na uwajibikaji kwa kuongeza kasi ya utoaji haki kwa kuimarisha matumizi ya tehama


‘’ umuhimu wa wadau wa Mahakama kujiandaa katika matumizi kamili ya Tehama kama daraja la utoaji haki Nchini,wadau wa Mahakama hasa wale wanaoshiriki uendeshaji wa Mashauri Mahakamani ,kama ofisi ya Taifa ya Mashitaka,ofisi ya wakili Mkuu wa serikali,chama cha mawakili Tanganyika na wananchi wote wenye mashauri Mahakamani,ni vema wakakumbuka kila mara kwamba Mahakama imedhamiria kupunguza na hatimaye kupunguza matumizi ya karasi,kuongeza uwazi na uwajibikaji kwa kuongeza kasi ya utoaji haki kwa kuimarisha matumizi ya tehama,jambo hili limekuwa likisemwa kuhusu dhamira ya mahakama katika matumizi kamili ya teknolojia hiyo ifikapo Mwaka 2025,manake katika hatua zote kuanzia usajili,usikilizwaji na utoaji wa hukumu Mahakama itumie teknolojia,amesema  jaji kiongozi Siyani

Mahakama imechukua hatua kadha wa kadha ikiwemo  usimikaji  wa mifumo mbalimbali  ya kielektroniki,lakini imeunganisha Mahakama kwenye mkongo ya Taifa,vitendea kazi mbalimbali vimenunuliwa ,kwa ujumla miundombinu mbalimbali imewekwa hata katika magereza zetu sehemu mbalimbali za Nchi yetu,  wote tujiandae mawakili wote wa kujitegemea na wale wa serikali wajue kwamba wakati umefika sasa wa kutumia teknolojia na kuachana na mazoea yale ya kwamba shahidi ni lazima afike Mahakamani  ,umwandae na kasha umwongoze akiwa mbele yako kumbe unaweza kufanya hivyo kwa kutumia teknolojia,kwa hiyo matarajio yetu ni kwamba wadau wetu wote wanaohusika na uendeshaji wa mashauri mahakamani hawatabaki nyuma na kwamba wataweka mipango na kuchukua hatua sawasawa na mahakama kuelekea matumizi ya tehama.’’ameeleza



Aliwataka mahakimu na mawakili kuwa na juhudi za pamoja  kuharakisha mchakato wa utoaji haki kama takwa la kikatiba ili  kupunguza au kuondokana kabisa  na mlundikano wa mashauri  ikiwemo  3419 yaliyopo katika ngazi mbali mbali za mahakama hapa Nchini.

‘’ni jukumu la wadau wetu kuhakikisha Mahakama inaondokana na Mlundikano wa mashauri , tunaposema mlundikano wa mashauri tunamaanisha  nini ? kwa Mahakama kuu shauri lolote ambalo limekaa zaidi ya miezi 24 ( kwa maana ya Miaka miwili )hili ni shauri linaitwa mlundikano kwa kuwa limekaa kwa muda mrefu ,kwa Mahakama za hakimu Mkazi na Wilaya shauri ambalo limekaa zaidi ya miezi  12 ( Mwaka mmoja ) hilo ni shauri la mlundikano,na kwa Mahakama za Mwanzo shauri ambalo limekaa kwa miezi sita,kwa hiyo ni wazi kwamba bado tunayo mashauri ya mlundikano Mahakamani, ameeleza

Hadi kufikia leo Novemba 21,2022 Mahakama kuu ya Tanzania ina ina jumla ya mashauri 1107 ya mlundikano,Mahakama za hakimu mkazi jumla ya mashauri 1129,na Mahakama za mwanzo mashauri 10,  huku Mahakama za watoto kuna jumla ya mashauri ya mlundikano 12,kwa hiyo kuna takribani jumla ya mashauri 3419 ya mlundikano kwenye mahakama za ngazi mbalimbali kuanzia Mahaka kuu ya Tanzania mpaka za chini .

’pamoja na jitihada mbalimbali  zinazoendelea kufanyika ili kuharakisha mchakato wa utoaji haki kama takwa la kikatiba,ni muhimu mawakili wasomi wasitumie mbinu za kiufundi kuchelewesha haki , wakati majaji na mahakimu wakichukua hatua mahsusi kuyasikiliza na kumaliza mashauri ya muda mrefu wadau na wadaawa wasiwe kikwazo,na badala yake waisaidie Mahakama kutimiza jukumu lake ,lakini namna nyingine bora ni mawakili kuwasaidia wadaawa kwa kuwawekea mazingira ya kupatana,wananchi watambue usuluhishi ni njia nzuri,na watumie fursa hiyo,matarajio ya Mahakama ni kuwa Mawakili wote na wasomi wa sheria nchini,watasaidia wananchi hususani wale wenye mashauri kuelewa umuhimu wa kuhakikisha haki inapatikana kwa wakati,kujenga desturi ya kutumia usuluhishi,na kutokuwa kikwazo kwa juhudi za  Mahakama kumaliza msongamano wa mashauri’’ amesema jaji kiongozi


Katika Mkutano huo jaji Mkuu wa Tanzania na  Mwenyekiti wa tume ya utumishi wa Mahakama Profesa Ibrahimu  Juma ameielezea  tume ya utumishi wa Mahakama kuwa ni chombo cha kikatiba kilichopewa mamlaka makubwa katika suala la  ajira ya majaji,mahakimu na watumishi wa Mahakama, na kwamba ndiyo mamlaka ya mwisho kwenye masuala ya nidhamu.

Ameeleza madhumuni ya ziara hiyo kwamba pamoja na mambo mengine imelenga kukutana na wenyeviti na wajumbe wa kamati za maadili za Mikoa na Wilaya ,pamoja na watumishi wa mahakama, lakini pia ni fursa nzuri ya kuitangaza tume hiyo kwa wadau.

Profesa Ibrahimu Juma alisema  katika ziara hiyo jumla ya Mahakama 18,za ngazi ya Wilaya zitazinduliwa katika maeneo mbalimbali Nchini Ikiwemo katika Wilaya za Busega na Itilima katika kanda ya Shinyanga ili kuongeza huduma za utoaji haki kwa wananchi

‘’Vile vile katika ziara hii tutapata nafasi ya kuzindua Mahakama za Wilaya mpya zipatazo 18,hii itafanyika Novemba 25, hii ni hatua kubwa kwa sabababu kuna maeneo mengi  yalikuwa na changamoto kubwa ya uhaba wa majengo,ulikuwa ukihitajika ukarabati mkubwa,kwa hiyo kwa muda wa miaka mitano tumekuwa tukishughulikia ujenzi ,kuhakikisha kila Wilaya Nchini Tanzania( wilaya 139)  zinapata Mahakama za kisasa kwa ngazi ya Wilaya ,ambapo  katika kanda ya Shinyanga tutazindua katika Wilaya za Busega na Itilima wilayani Simiyu (Mkoa wa Simiyu  unahudumiwa na Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga)’’alisema profesa Ibrahimu Juma

 

Awali jaji mfawidhi wa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga Athuman   Matuma amesema Mahakama hiyo imekuwa na tija na ufanisi kutokana na ushirikiano mzuri kutoka kwa wadau mbalimbali

‘’katika Mkoa wa Shinyanga imekuwa ikipata ushirikiano mkubwa sana katika utendaji wa majukumu yake na shughuli za kila siku kutoka kwa wadau ,ambao ni muhimu zaidi katika kuisaidia  Mahakama kutekeleza majukumu yake ya utoaji wa haki na hivyo kuimarisha utendaji haki nchini,Mahakama ya Tanzania iliweka mpango ya kuratibu utekelezaji wa ushiriki wa wadau katika mpango mkakati wake uliopita wa 2015/2016 mpaka 2019/2020,ambapo ilifanikiwa kupata ushirikiano wa kutosha ,na hivyo kutekeleza majukumu yake ya utoaji haki ipasavyo.

Vilevile katika mpango mkakati wa sasa wa 2020/2021  mpaka 2022/2025 tumeweka mikakati ,vipaumbele na malengo mbalimbali ili kuimarisha ushirikiano na wadau.

Ameshukuru na kupongeza ofisi ya taifa ya Mashtaka NBS na chama cha wanasheria wa kujitegemea Tanganyika Law Society kwa ushirikiano wao katika ufunguaji wa mashauri kwa njia ya mtandao,licha ya kuwepo changamoto kadhaa za kimtandao,ambapo kwa sasa katika Mkoa wa Shinyanga mashauri yote ya jinai kutoka ofisi ya taifa ya mashtaka na mashauri yote ya madai kutoka kwa wanasheria wa kujitegemea yanafunguliwa kwa njia ya mtandao.

Ameshukuru pia ofisi ya upelelezi ya makosa ya jinai  Mkoa wa Shinyanga  kwa kukamilisha upelelezi kwa wakati ikiwa ni pamoja na mashauri ya mauaji ,kwa sasa takribani mashauri 130 yamekamilika upelelezi wake ambapo yanasubiri kusikilizwa katika vikao vya Mahakama kuu.

Ameishukuru pia ofisi ya taifa ya mashtaka kwa kushirikiana vizuri na ofisi ya upelelezi wa makosa ya jinai  katika kukamilisha upelelezi wa makosa ya jinai ikiwemo mashauri ya mauaji,ambapo ameishukuru pia ofisi ya taifa ya mashtaka kwa kutoa ridhaa kwa wakati kwa mashauri ambayo usikilizaji wake unahitaji ridhaa za Mkurugenzi wa mashtaka,hali kadharika ameishukuru ofisi ya mashitaka Shinyanga kwa ushirikiano wao katika kufanya jukumu lao la msingi la uendeshaji wa mashtaka kwa kuzingatia ratiba za mashauri,kuhudhuria na kushiriki kikamilifu katika vikao vya awali kabla ya usikilizaji wa mashauri (pre- sessions) na vikao vya usikilizaji wa mashauri (sessions) kwani bila waendesha mashtaka mashauri mengi ya jinai hayawezi kusonga mbele,kwa hiyo wamesaidia kwa kiwango kikubwa Mahakama kufikia katika malengo iliyojiwekea ya kusimamia utendaji wa haki.

Amewashukuru wazee wa Mahakama pamoja na viongozi wote wa dini ambao wana mchango  na jukumu kubwa la  kujenga  maadili katika jamii  ili  iweze kuepuka    kutenda makosa ya jinai na   hata kujiepusha na migogoro inayozua mashauri ya madai,kufanya usuluhishi wa mogoro ya ndoa kabla ya kufikishwa mahakamani kama inavyoelekeza sheria,na kwamba wameendelea kutoa ushirikiano wa kutosha  kwa  Mahakama hivyo kusaidia kuirahisishia wa kutekeleza majukumu yake.

Kwa upande wake jaji wa mahakama ya rufani na kamishna wa tume ya utumishi wa mahakama Dkt. Geraid Ndika amewataka wajumbe wa kamati za maadili  za Mkoa na Wilaya kutunza siri za vikao vya kamati pamoja na taarifa za kamati.

Mheshimiwa jaji Dkt. Ndika amezitaja baadhi ya changamoto zinazojitokeza wakati wa utekelezaji wa majukumu ya kamati za maadili za Mkoa na wilaya kuwa ni pamoja na uelewa mdogo wa wananchi juu ya aina ya malalamiko yanayopaswa kuwasilishwa kwenye kamati na uwepo wa kamati ili waweze kuzitumia, na kwamba changamoto nyingine ni kamati kutokutana kama ilivyoelekezwa na sharia kwa kigezo cha ufinyu wa bajeti lakini pia mabadiliko ya mara kwa mara ya wenyeviti wa kamati na baadhi ya kamati kutowasilisha kwa tume ripoti za vikao vyao.

Amesema ni muhimu zaidi wajumbe wa kamati kuzingatia muongozo wa uendeshaji wa kamati za maadili hatua ambayo itadumisha nidhamu na kuimarisha utendaji wa haki Nchini.

Post a Comment

Previous Post Next Post