Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Wananchi wa Mkoa wa Shinyanga wametakiwa
kufuata taratibu za kisheria wakati wote wanapotafuta haki ama suluhu kwenye mashauri ya kijamii na
kifamilia, ili kuondokana na migogoro ikiwemo migogoro ya ardhi, ndoa pamoja na
masuala ya mirathi.
Hayo yamezungumza na Mwenyekiti wa kamati ya
huduma ya msaada wa kisheria Mkoa wa Shinyanga Bwana John Shija kwenye kilele cha
maadhimisho ya wiki ya huduma ya msaada wa kisheria ambayo kimkoa imefanyika
katika kata ya Masanga Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga.
Mwenyekiti huyo amewasisitiza wananchi kuepuka
migogoro na kwamba pale inapotokea wanapaswa kufuata taratibu za kisheria ili
kupata haki zao.
“Ni
kosa kisheria kuvunja ndoa nje ya mahakama chombo pekee kinachovunja ndoa ni
mahakama ni kosa kisheria kugawana mali za mirathi bila kufika mahakamani
unaweze kushtakiwa na ukatiwa hatiani na ukafungwa, kuna suala la migogoro ya
ardhi tusigombane pale unapoona kuna mgongano mmeingiliana kwenye mpanga ama
ardhi utaratibu wa kisheria unaeleweka nenda kwenye baraza la kata”
“Niwasihi
kwamba tufuate taratibu za kisheria ili tutunze amani tuwe na upendo sheria
zimekuja kwa ajili ya kutunza amani kunyosha njia ya migogoro ili watu waishi
kwa amani badala ya kushikana mapanga na kuanza kupigana na nimarufuku mwanamke
aliyefiwa na mume kuondolewa kwenye ardhi bila kufuata utaratibu wa kisheria”.amesema Mwenyekiti John Shija
Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia
Kwesigabo pamoja na mambo mengine amewataka wananchi kuepuka ukatili wa
kijinsia huku akiwasisitiza wazazi na walezi kutimiza wajibu wao kwa watoto ili
waweze kufikia ndoto zao.
Aidha afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Shinyanga
Lydia Kwesigabo amesisitiza wananchi kutofumbia macho ukatili unaofanyika
kwenye familia na kwamba wanapaswa kutoa taarifa za matukio ya ukatili ili
hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa.
“Ukatili
ni matendo yanayomzalilisha mtu, yapo
matendo sisi wazazi tunawafanyia watoto tukiamini kwamba ni adhabu kumbe tunawafanyia ukatili leo hii mototo
kafanya kosa unakwenda kuchukua chombo
cha moto unamchoma sehemu za mwili wake
unasababisha majeraha hivi hapo harasa ni ya nani kwahiyo wazazi tuache
kuwafanyika ukatili watoto tujitahidi kutimiza wajibu wetu kwa kuhakikisha
tunamlinda mototo na kuwakagua mara kwa mara hasa watoto wa kike”.
“Upande
wa madhara moja wapo ni mimba za utotoni tunaona kwamba watoto ambao wapo shule
wanapoteza mwelekeo kwa sababu ya kupata mimba lakini madhara mengine ni
ulemavu kama wanandoa watakatana mapanga mmoja wapo atapata ulemavu lakini pia
vifo tunasikia hata kwenye vyombo vya habari mara nyingi tunasema unapokuwa na
hasira usichukue maamuzi magumu unapaswa utulie kwanza mwisho wa siku utachukua
maamuzi ambayo niya hekima lakini pia kuna kupata magonjwa kwa mfano mtu
amebakwa huwezi kumjua aliyekubaka kama atakuwa salama anaweza kuwa ana maambukizi
ya magonjwa”.amesema
afisa ustawi wa jamii Lydia
“Tunaombeni
ushirikiano kwa hao watu wanaofanya matukio ya ukatili wapo watu wanaona kabisa
mtu anafanyiwa ukatili lakini wanaogopa kutoa taarifa kumbuka unakuwa
unamkosesha haki mtu aliyefanyiwa ukatili yapo maeneo mengi ya kuripoti matukio
ya ukatili kwa mfano kwa watoto shule unaweza kuripoti kwa mwalimu au ofisi za
kata na ngazi zingine lakini pia ukiona huwezi au huwaamini piga simu sisi
tunatunza siri yako ilikumuokoa yule mtu anayefanyiwa ukatili kwahiyo tusikae
kimya tutoe taarifa kuna zile namba za serikali ambazo zinatumika bure kwahiyo
na sisi kwenye ukatili tunatumia namba 116 piga hii namba ili kutoa taarifa ya
ukatili”.amesema Lydia
Afisa wa taasisi ya kuzuia na kupambana na
rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Kishapu Adam Mwihechi ametumia nafasi hiyo kuwaomba
wananchi kuepuka kushiriki vitendo vya rushwa na kwamba kila mwananchi anawajibu
wa kushirika katika kuzuia na kupambana na rushwa.
“Kila
mwananchi anajukumu la kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa TAKUKURU au kwa
vyombo vyingine vya sheria au dola, mwananchi unatakiwa kuichukia rushwa na
kuepuka kushiriki vitendo vya rushwa kumbuka rushwa ni kikwazo kikubwa kwa
demokrasia, utawala bora, haki za binadamu na ni tishio kwa amani, utulivu na
usalama katika jamii wewe ndiye unayeathirika zaidi katika kila tendo la rushwa
unaloshiriki hivyo amka acha mara moja rushwa”.amesema Adam Mwihechi
Wakili wa serikali ofisa ya Taifa ya mashtaka Mkoa
wa Shinyanga Rose Kimaro amezungumzia suala la dhamana huku akiwasisitiza
wananchi kutoa ushahidi kwa mtuhumiwa au mshtakiwa ili kuondoa changamoto.
“Dhamana
hii huwa inatolewa kwa makosa ya jinai pale ambapo mtuhumiwa yupo katika
kizuizi cha polisi au kizuizi cha mahakama na dhamana ni haki ya kikatiba wala siyo upendeleo, katika kesi zetu
tunazoendesha ni pamoja na kesi za ukatili wa kijinsia”
“kumekuwa
na changamoto mbalimbali kwamba mashahidi hawafiki mahakamani kwahiyo hapo
tunakuwa tunakosa ushahidi wa kuendeleza ile kesi na yule mhanga anashindwa
kupatiwa haki yake kwahiyo mnatakiwa muonyeshe ushirikiano kuanzia kwenye
upelelezi katika ngazi ya polisi na shauri linapofikishwa mahakamani basi muonyeshe
ushirikiano kwetu kwa kuja mahakamani kutoa ushahidi ili tuweze kushinda kesi”.amesema wakili Rose Kimaro
Kwa
upande wake Mwanasheria wa kituo cha msaada wa kisheria Mkoa wa Shinyanga
Andrew Jeremiah ametoa elimu kwa wananchi,kuhusu namna bora ya kutafuta utatuzi
wa migogoro ambapo amewasihi kufikisha changamoto ama migogoro sehemu husika
ili ziweze kutatuliwa katika utaratibu mzuri uliowekwa.
Nao baadhi ya wananchi wa kata ya Masanga
waliohudhuria kwenye kilele cha maadhimisho ya wiki ya huduma ya kisheria
wamepongeza huku wakishukuru kwa kupata elimu hiyo.
Aidha baadhi ya wananchi waliohudhuria katika
maadhimisho hayo wamepata nafasi ya kuuliza maswali mbalimbali wakitaka kuelewa
zaidi juu ya masuala ya kisheria ambapo timu ya wataalam kutoka Mkoa na wilaya
wamejibu maswali hayo papo kwa hapo.
Moja ya maswali yaliyoibuliwa katika
maadhimisho hayo ni pamoja na migogoro ya ardhi, migogoro ya ndoa, umiliki wa
ardhi, masuala ya mirathi, masuala ya dhamana mahakamani, upatikanaji na utoaji
wa talaka, makosa ya ukatili wa kijinsia ikiwemo ubakaji, ulawiti, vipigo
pamoja na ushirikiana.
Wiki ya maadhimisho ya huduma ya msaada wa
kisheria Mkoa wa Shinyanga ilizinduliwa katika kata ya Mwakipoya Novemba 8,2022
na kilele chake kimefanyika kwenye kijiji cha Bulekela kata ya Masanga Novemba 12 ambapo mgeni
rasmi katika kilele hicho alikuwa afisa
wa huduma za kisheria Wilaya ya Kishapu Bwana Benard Kadanda.
Maadhimisho ya wiki ya huduma za kisheria ni
huduma inayotolewa kwa lengo la kuibua matatizo ya ukatili wa kijinsia dhidi ya
wanawake, watoto, wazee, walemavu na wanaume Nchini.
Wiki ya huduma ya msaada wa kisheria hufanyika
kila Mwaka kwa lengo la kutoa elimu kwenye jamii ili kuwa na uelewa kuhusu
masuala ya kisheria ambapo kwa Mwaka huu 2022 maadhimisho ya wiki ya huduma za
kisheria katika mkoa wa Shinyanga umefanyia maadhimisho hayo kwenye wilaya ya
Kishapu kwa kauli mbio isemayo “UKATILI NA UDHALILISHAJI WA KIJINSIA NI KIKWAZO
CHA MAENDELEO YA TAIFA WANANCHI WOTE TUSIMAME PAMOJA KUZUIA”
Mwenyekiti wa kamati ya huduma ya msaada wa kisheria Mkoa wa Shinyanga Bwana John Shija akizungumza na wananchi kwenye kilele cha maadhimisho hayo
Aliyenyosha mikono juu ni Mwenyekiti wa kamati ya huduma ya msaada wa kisheria Mkoa wa Shinyanga John Shija akiwasisitiza wananchi kufuata utaratibu wa kisheria ili kuzuia migogoro mbalimbali
Mgeni rasmi katika kilele hicho afisa wa huduma za kisheria Wilaya ya Kishapu Bwana Benard Kadanda akizungumza na wananchi
Afisa ustawi wa jamii Mkoa wa Shinyanga Lydia Kwesigabo akizungumza katika kilele cha maadhimisho hayo
Afisa wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Kishapu Adam Mwihechi akitoa elimu kwa wananchi
Wakili wa serikali ofisa ya Taifa ya mashtaka Mkoa wa Shinyanga Rose Kimaro akitoa elimu kwa wananchi
Mwanasheria wa kituo cha msaada wa kisheria Mkoa wa Shinyanga Andrew Jeremiah akitoa elimu kwa wananchi
Diwani wa kata ya Masanga Mh: Enock Reuben akipongeza maadhimisho hayo kufanyika katika kata yake
Post a Comment