" ASKOFU BUGOTA AWAKUMBUSHA WAKRISTO MAMBO YA MSINGI KUELEKEA NYAKATI ZA KUZALIWA KWA YESU

ASKOFU BUGOTA AWAKUMBUSHA WAKRISTO MAMBO YA MSINGI KUELEKEA NYAKATI ZA KUZALIWA KWA YESU

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Askofu wa makanisa ya Africa Inland Church Tanzania (AICT)  Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota amesema changamoto za maisha hutengeneza aibu kwa kila mtu hivyo amewataka wakristo kufanya kazi kwa bidii ili kuimarisha uchumi wa mtu mmoja mmoja.

Ameyasema hayo wakati akihubiri kwenye ibada ya Jumapili katika kanisa la AICT Kambarage mjini Shinyanga ambapo amewakumbusha wakristo kufanya kazi, kuondoa uvivu pamoja na kumtanguliza Mungu katika maisha ya kila siku.

Askofu Bugota ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wakristo wote kujenga utaratibu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo na  kufanya maombi  ya  kuombea kizazi cha ulimwengu huu ili kukua katika maisha yanayompendeza Mungu.

 “Mungu ametubariki kwa neema yake tunapokuwa kwenye maoni ni muhimu sana  kukiombea kizazi ili uzao uwe na baraka jumuishi, mimi ninaamini maombi tunayofanya Mungu ataleta matokeo na  majibu yake yatakuwa na baraka ambazo zitawagusa wengine”.

“Unapobarikiwa maana yake unatakiwa uwaombee na wengine wapate hizo baraka majibu ya Bwana lazima yatengeneze furaha na shangwe ambazo zitatengeneza baraka za jumla katika maisha”.amesema Askofu Bugota

Askofu Bugota amewakumbusha wakristo wote na jamii kwa ujumla kuacha dhabi na  kumrudia Mungu hasa nyakati hizi kuelekea kuzaliwa kwa Yesu  kristo ili aweze kujibu mahitaji ya kila mtu.

Askofu wa makanisa ya Africa Inland Church Tanzania (AICT)  Dayosisi ya Shinyanga Zakayo Bugota akihubiri kwenye ibada ya Jumapili leo Desemba 18,2022.

Waumini wakisikiliza mahubiri katika ibada ya Jumapili 



Post a Comment

Previous Post Next Post