Jeshi la Wananchi wa
Tanzania Mkoa wa Shinyanga leo limeadhimisha Miaka 61 ya Uhuru wa Tanganyika
kwa kushiriki katika shughuli mbali mbali za kijamii ikiwemo upandaji wa miti
na usafi wa mazingira katika maeneo mbali mbali ya Manispaa ya Shinyanga
Mkuu wa vikosi vya Jwtz
kanda ya Shinyanga kanali Machuza Alex Sunzu amesema askari wa Jeshi hilo
wameadhimisha siku hii kwa kupanda miti 400 katika maeneo mbalimbali ya
Manispaa ya Shinyanga na kwamba maadhimisho hayo yalianza tangu Disemba 02,kwa
kushiri katika shughuli za usafi wa mazingira katika maeneo mbali mbali ikiwemo
kwenye taasisi za serikali kwa kushirikiana na Wananchi
Akizungumza
baada ya kupanda miti hiyo afisa wa jeshi la wananchiwa Tanzania Jwtz, meja Ndyamkama
kente amewaomba wakazi wa Shinyanga kutunza miti iliyopandwa ili kuhifadhi mazingira
Kwa upande wake Afisa
maliasili na mazingira wa Manispaa ya Shinyanga Bwana Ezra Manjerenga, ambaye
ameshirikiana na askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania kanda ya Shinyanga
amesema lengo la kupanda miti katika
siku ya kumbukumbu ya Uhuru ni kuhakikisha uhuru unadumishwa katika mazingira
safi na salama
Leo Disemba 09,2022
watanzania wameadhimisha kumbukumbu ya Miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania
Bara,ambapo Mkoa wa Shinyanga umeadhimisha kwa namna mbalimbali ikiwemo kufanya
midahalo, makongamano na kushiriki katika shughuli za kijamii ikiwemo kupanda
miti na usafi wa mazingira.
Mkuu wa vikosi vya Jwtz kanda ya Shinyanga kanali Machuza Alex Sunzu.
afisa wa jeshi la wananchiwa Tanzania Jwtz, meja Ndyamkama kente.
Afisa maliasili na mazingira wa Manispaa ya Shinyanga Bwana Ezra Manjerenga
Post a Comment