" KIKUNDI CHA JAMII MPYA MAMA YANGU, NCHI YANGU KIMETOA MSAADA KWA WATOTO BUHANGIJA MJINI SHINYANGA

KIKUNDI CHA JAMII MPYA MAMA YANGU, NCHI YANGU KIMETOA MSAADA KWA WATOTO BUHANGIJA MJINI SHINYANGA

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Kikundi cha Jamii mpya Mama yangu, Nchi yangu Mkoa wa Shinyanga  kimetoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija jumuishi  kufuatia  Bweni la shule hiyo kutetekea kwa moto Novemba 22 Mwaka huu 2022.

Vitu vilivyotolewa na kikundi cha Jamii mpya  ni pamoja na sabuni, miswaki, dawa ya meno, Dofi, Juice pamoja na Biscut kama hatua ya kusaidia kituo hicho ambacho kinauhitaji wa vitu mbalimbali baada ya kutokea kwa ajali hiyo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo mratibu wa kikundi cha Jamii mpya  Mkoa wa Shinyanga Bwana Leonard Maige amesema msaada huo ni sehemu ya kikundi hicho kuwafariji wanafunzi wa shule hiyo baada ya kupatwa na tukio hilo.

“Tulipokea kwa maskitiko makubwa tukio lililotokea hapa shuleni na kusababisha Bweni kuungua moto ambapo watoto watatu walifariki Dunia  sisi kama jamii mpya Mkoa wa Shinyanga tunatoa vitu baadhi vichache kwa ajili ya kuwashika mkono na sisi tumeguswa na ndiyo maana nimeamua tuje tuwape hiki tulichonacho”.amesema Mratibu Leonard Maige

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo Mwalimu wa shule ya msingi Buhangija Mashinde Daudi amekishukuru kikundi cha Jamii mpya mama yangu, Nchi yangu kwa kuguswa na tukio hilo.

Kwa niamba ya stafu shule ya msingi Buhangija tunawashukuru sana kikundi cha Jamii mpya kwa kuwa pamoja na hawa watoto kwa kuguswa kuja kutoa hivi vitu ambavyo vitasaidia kupunguza changamoto”.amesema Mwalimu Mashinde Daudi

Watu mbalimbali wameendelea kupeleka msaada wa aina mbalimbali kwa wanafunzi wa Bweni wa shule ya msingi Buhangija jumuishi kama hatua ya kusaidia mahitaji baada ya Bweni moja la wanafunzi wa kike kuungua na kuteketeza magodoro, vitanda na vifaa vya shule.

Jamii mpya ni kundi la kizalendo kwa Taifa, serikali na chama cha mapinduzi ambacho kinafanya kazi chini ya ofisi ya mkuu wa Mkoa, mkuu wa Wilaya na wakurugenzi wa Halmashauri kwa kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo, kijamii, elimu na kuhamasisha vijana na wanawake kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi.

Aidha kikundi cha Jamii mpya kinafanya kazi kupitia kampeni ya kitaifa ijulikanayo kama MAMA YANGU, NCHI YANGU na kwamba kilianzishwa Mwaka 2018 chini ya mawaziri, wakuu wa Mikoa na wakurugenzi kwa lengo la kuunganisha makundi ya vijana, wanawake na wanaume ili kwa pamoja kushiriki shughuli za uzalishaji mali, uchumi na mambo ya kijamii na kuweza kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mratibu wa kikundi cha Jamii mpya  Mkoa wa Shinyanga Bwana Leonard Maige akizungumza kwenye hafla hiyo

Katibu wa kikundi cha Jamii mpya Mama yangu, Nchi yangu Mkoa wa Shinyanga Bi. Selina Leonce Kimola akizungumza kabla ya kukabidhi msaada huo.

Baadhi ya wanakikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika mazungumza ya pamoja kabla ya kukabidhi msaada kwa watoto wenye uhitaji shule ya msingi Buhangija.

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakisalimiana na baadhi ya watoto wanaosoma shule ya msingi Buhangija Manispaa ya Shinyanga.

Baadhi ya wanachama wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakiendelea kusalimiana na baadhi ya watoto wanaosoma shule ya msingi Buhangija Manispaa ya Shinyanga.
mratibu wa kikundi cha Jamii mpya  Mkoa wa Shinyanga Bwana Leonard Maige akisalimiana na mmoja wa wanafunzi wanaosoma katika shule ya msingi Buhangija.

Wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija wakipokea vitu mbalimbali vilivyoletwa na kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga



Baadhi ya viongozi na wanachama wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga kabla ya kukabidhi msaada huo.
Baadhi ya viongozi na wanachama wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakiwa kwenye picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Buhangija baada ya kukabidhi msaada huo.



Zoezi la kugawa msaada wa vitu mbalimbali likiendelea kwa watoto wenye uhitaji wa shule ya msingi Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga 

Zoezi la kugawa msaada wa vitu mbalimbali likiendelea kwa watoto wenye uhitaji wa shule ya msingi Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga 
Zoezi la kugawa msaada wa vitu mbalimbali likiendelea kwa watoto wenye uhitaji wa shule ya msingi Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga 



Zoezi la kugawa msaada wa vitu mbalimbali likiendelea kwa watoto wenye uhitaji wa shule ya msingi Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga 



Zoezi la kugawa msaada wa vitu mbalimbali likiendelea kwa watoto wenye uhitaji wa shule ya msingi Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga 


Zoezi la kugawa msaada wa vitu mbalimbali likiendelea kwa watoto wenye uhitaji wa shule ya msingi Buhangija iliyopo Manispaa ya Shinyanga 

















Baadhi ya viongozi wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakienda kuangalia Bweni lililoteketea kwa ajali ya Moto shule ya msingi Buhangija Manispaa ya Shinyanga 


Baadhi ya viongozi wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakienda kuangalia Bweni lililoteketea kwa ajali ya Moto shule ya msingi Buhangija Manispaa ya Shinyanga 



Baadhi ya viongozi na wanachama wa kikundi cha jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakiendelea na zoezi la kuangalia Bweni lililoteketea moto shule ya msingi Buhangija.



Baadhi ya viongozi na wanachama wa kikundi cha jamii mpya Mkoa wa Shinyanga wakiendelea na zoezi la kuangalia Bweni lililoteketea moto shule ya msingi Buhangija.
















Viongozi mbalimbali na wanachama wa kikundi cha Jamii mpya Mama yangu, Nchi yangu Mkoa wa Shinyanga wakiwa katika  picha ya pamoja kwenye ubao wa shule ya msingi Buhangija baada ya kutoa msaada kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Upande wa kulia ni Mratibu wa kikundi cha Jamii mpya  Mkoa wa Shinyanga Bwana Leonard Maige wakiwa kwenye picha ya pamoja na katibu wa kikundi cha Jamii mpya Mkoa wa Shinyanga Bi.Selina Kimola.

Post a Comment

Previous Post Next Post