" VITUO VYA TAARIFA NA MAARIFA VYATATHIMINI MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI, WAZAZI NA WALEZI WAHIMIZWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

VITUO VYA TAARIFA NA MAARIFA VYATATHIMINI MAADHIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI, WAZAZI NA WALEZI WAHIMIZWA KUTIMIZA WAJIBU WAO

 Na Stela Paul Shinyanga

Wazazi na walezi wamehimizwa kutekeleza na kusimamia vyema majukumu yao ya msingi kwa watoto wanaosoma shule za Msingi na Sekondari ikiwa ni pamoja na kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni ili  kuongeza ufaulu  pamoja na kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia vinavyofanywa dhidi yao..

Wito huo umetolewa  Disemba 10,2022 na Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Mhe. Andason Mandia   wakati wa  Kikao cha Tathimini  cha Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia kilichoandaliwa na Vituo vya Taarifa na Maarifa  vinavyowezeshwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania TGNP.

Amesema wazazi na walezi wanawajibu wa kuhakikisha watoto wanapata huduma zote muhimu wanapokuwa shuleni.

"Watoto wetu tumekuwa tukiwakatili hawali chakula shuleni, tafisiri ya elimu bila malipo inamaanisha hakuna kulipa ada na vile ambavyo tulikuwa tukilipia kama wazazi, lakini mzazi unawajibu wa kumhudumia mtoto akiwa shuleni" Amesema Mhe. Andason.

"Kwahiyo niombe wazazi ni jukumu letu la msingi kuhakikisha yale mahitaji muhimu kwa mtoto unashiriki kikamilifu ikiwemo chakula mashuleni" Amesema Mhe. Andason.

Kwa upande wake Katibu wa Vituo vya Taarifa na Maarifa Wilaya ya Kishapu Bwana Peter Nestory amesema wamefanikiwa kuelimisha jamii juu ya ukatili wa kijinsia kupitia mikutano ya hadhara pamoja na midahalo mbalimbali.

"Tumetoa elimu kupitia mikutano ya hadhara, kuendesha midahalo, kutoa elimu ya kijinsia shuleni kwa wanafunzi ambao wamekuwa wahanga wa vitendo vya ukatili na hivyo kubaini kwamba Watoto wengi wamekuwa wakibakwa , kulawitiwa, kupata mimba za utotoni na kusababisha watoto kupoteza ndoto zao na jamii kumaliza kesi kindugu" Amesema Bwana Peter.

Kwa upande wake Mratibu wa Vituo vya Taarifa na maarifa          Bi.Fredina Saidi ameitaka jamii kuendelea kutoa taarifa za vitendo vya ukatili na kuwafichua watu wanaofanya vitendo hivyo ili kujenga ustawi wa jamii na watoto kufikia ndoto zao

"Niwaombe mtoe taarifa ambazo zitasaidia kutokomeza ukatili lengo letu ni kuwa na jamii salama. Pia hata watoto wafikie ndoto zao maana msipotoa na kufichua vitendo vya ukatili vitaendelea kuleta athari katika jamii"Amesema Bi. Fredina.

 Nae Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya Ya Kishapu Bwana Joseph Swalala amewataka wadau wa kikao hicho kuwa mstari wa mbele kusimamia maadhimio  ya kikao ili kufikia malengo ya kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii.

"Popote tunapokuwa tuongelee ajenda ya ukatili, tumeadhimia watoto wapate chakula shuleni kwahiyo tuhakikishe shule zinapofunguliwa watoto wanaanza kupata chakula, wazazi na walezi kuwajibika katika suala la malezi hivyo tutaendeleza kushirikiana kupinga ukatili" Amesema Bwana Swalala

Baadhi ya wananchi waliohudhuria kikao hicho wameahidi kuwa mabalozi katika kuelimisha jamii nyingine na kwamba wanaunga mkono maadhimio ya kikao ikiwemo suala la watoto kupata chakula shuleni.

Disemba 10, 2022 Vituo vya taarifa na maarifa Wilaya ya Kishapu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa kupinga ukatili wa kijinsia wamefanya kikao cha Tathimini ya kilele cha maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia.

Kaimu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapi Mhe. Andason Mandia akitoa hotuba katika kikao cha Tathimini ya Maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatiliMratibu wa vituo vya taarifa na maarifa wilaya ya kishapu Bi. Fredina Saidi akizungumza

 

katibu wa vituo vya taarifa na maarifa wilaya ya kishapu Bwana peter Nestory akisoma taarifa ya utekelezaji 

Afisa Maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Bwana Joseph Swalala akizungumza wakati wa kikao

Post a Comment

Previous Post Next Post