Viongozi wakiongozwa na Afisa Elimu Mkoa, Naibu Meya,
Katibu wa Mbunge, Mdhibiti Mkuu wa Ubora pamoja na Mwl. Makoye wakikata keki
kwa pamoja kuadhimisha umoja wa walimu katika sherehe za Mei Mosi.
Walimu wa shule za sekondari katika Manispaa ya
Shinyanga wameadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) kwa sherehe
maalum iliyofanyika Mei 1, 2026 katika viwanja vya Family Park, ikiwa na lengo
la kuwatambua na kuwapongeza kwa mchango wao katika sekta ya elimu.
Sherehe hiyo iliandaliwa na Afisa Elimu Sekondari wa
Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Richard Makoye, ambaye pia ni mfanyakazi bora wa
mwaka 2026 katika manispaa hiyo.
Kauli mbiu ya sherehe hiyo ni “Sisi Wote ni
Watumishi Bora” iliwakutanisha walimu mbalimbali ambapo walipata fursa ya
kula, kunywa na kuburudika kupitia muziki, burudani za moja kwa moja pamoja na
shughuli mbalimbali ikiwemo upigaji picha za pamoja.
Miongoni mwa matukio yaliyovutia zaidi ni mashindano
ya kumtafuta Miss Teacher na Mr Teacher, ambapo washindi waliibuka na zawadi
nono. Katika mashindano hayo, taji la Miss Teacher lilinyakuliwa na Madam Nurah
Kamuntu ambaye ni Mkuu wa Shule ya
Sekondari Shinyanga Girls, huku Mr Teacher akiibuka kuwa Mwalimu Seif Juma wa
Shule ya Sekondari Busulwa ambaye pia ni Katibu wa Michezo wa Manispaa ya
Shinyanga.
Timu ya majaji wa mashindano hayo iliongozwa na Afisa
Michezo wa Manispaa ya Shinyanga, Bw. Arnold Lukiza.
Mgeni rasmi katika sherehe hiyo alikuwa Afisa Elimu wa
Mkoa wa Shinyanga, Mwl. Samson A. Hango, ambaye aliwapongeza walimu kwa kazi
kubwa wanayoifanya na kuwataka kuendelea kujituma ili kuinua kiwango cha elimu
kwa wanafunzi wa Tanzania. Aidha, aliwapongeza viongozi wa elimu kwa ubunifu wa
kuandaa tukio hilo.
Kwa upande wake, Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga,
Mhe. Pendo Sawa, alisema tukio hilo ni la kipekee kwani limewawezesha walimu
kukutana na kusherehekea mafanikio yao, akipendekeza liwe linafanyika kila
mwaka.
Wageni wengine wa heshima waliohudhuria ni pamoja na
Katibu wa Mbunge, Bw. Samwel Jackson, Mdhibiti Mkuu wa Ubora wa Elimu Mkoa Bi.
Edith Kaijage, Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa Charles Luchagula, madiwani pamoja
na viongozi mbalimbali.
Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl.
Richard Makoye, ambaye pia ni mfanyakazi bora wa mwaka 2026 katika manispaa
hiyo alipongezwa kwa maandalizi mazuri ya tukio hilo lililowaleta pamoja walimu
katika mazingira ya furaha na mshikamano.
Afisa Elimu wa Mkoa wa Shinyanga, Mwl. Samson A. Hango, akizungumza na walimu wakati wa maadhimisho ya Mei Mosi yaliyofanyika Family Park, Shinyanga.
Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Pendo Sawa, akitoa salamu na kuwapongeza walimu kwa mchango wao katika sekta ya elimu wakati wa sherehe hizo.
Washindi wa Miss Teacher wakiwa katika picha ya pamoja na Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Richard Makoye, mara baada ya kutangazwa washindi katika sherehe za Mei Mosi.
Washindi wa Miss Teacher wakiwa katika picha ya pamoja na Afisa Elimu Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Richard Makoye, mara baada ya kutangazwa washindi katika sherehe za Mei Mosi.

Washindi wa Miss Teacher na Mr Teacher wakiwa katika picha ya pamoja na majaji mara baada ya kutangazwa rasmi kuwa washindi.

Mkuu wa Mkoa
wa Shinyanga Mhe. Mboni Mhita, akimkabidhi cheti cha mfanyakazi hodari Afisa Elimu
Sekondari wa Manispaa ya Shinyanga, Mwl. Richard Makoye kwenye sherehe za Mei
Mosi kimkoa.
SHY TALENT FILMS - CONTENT YA MWISHO DRAMA
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Wasiliana nasi:
📍 East African Spirits (T) Ltd
📞 +255 767 650 806 | +255 652 096 254






Post a Comment