Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Joseph Mkude amewashauri watumishi
wa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga kufanya kazi kwa weledi ikiwa ni
pamoja na kufuata sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ya utumishi wa umma.
Akizungumza kwa niamba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga
kwenye uzinduzi wa wiki ya kisheria yanayofanyika kwenye uwanja wa Zimamoto
Nguzonane mjini Shinyanga.
DC Mkude pamoja na mambo mengine ametumia nafasi
hiyo kuwaomba wananchi na wadau mbalimbali kujitokeza ili kunufaika na fursa
hiyo huku akiwasisitiza watumishi wa Mahakama kuzingatia maadili ya utumishi wa
umma na kwamba wananchi waweze kupata haki zao.
“Nawaomba
wananchi ambao hawajabahatika kufika kwenye viwanja hivi kwa leo kujitokeza ama
kushirikia kikamilifu katika wiki hii ya sheria kwani maonsho na utoaji elimu
juu ya maswala mbalimbali ya kisheria yataendeleo kutolewa hadi tarehe moja mwezi wa pili 2023 pia napenda kuwahimiza wananchi kuitumia
mahakama katika kutafuta haki zao kwani ndicho chombo pekee chenye mamlaka ya
mwisho katika utoaji wa haki Nchini”.
“Napenda
kutoa wito kwa watumishi wa Mahakama kufanya kazi kwa weledi kwa kuzingatia
maadili ya utumishi wa umma sheria, kanuni na miongozo mbalimbali ya utumishi
wa umma”.amesema DC Mkude
Kwa upande wake Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu ya
Tanzania kanda ya Shinyanga Athumani Matuma amesema lengo la maadhimisho hayo
ni kutoa elimu kwa wananchi juu ya shughuli mbalimbali zinazotolewa na
Mahakama.
“Malengo
ya maadhimisho haya ni kutoa elimu kwa upana kwa wananchi juu ya shughuli
mbalimbali zinazotolewa na Mahakama na maboresho yanayoendelea kufanyika ndani ya
Mahakama lakini vile vile tunaendelea tunakuwa tunawashirikisha wadau wetu wa
Mahakama ambao nao wanapata fursa ya kutoa elimu na mara nyingi shughuli hizo
ambazo wanazitoa wakati mwingine zinapelekea uwepo wa migogoro na mashauri
Mahakamani kwahiyo tukitumia fursa hii
ya wiki ya kisheria kwa kupata elimu sahihi kunauwezekano mkubwa tukaziepuka
migogoro mingi”.amesema Matuma
Leo umapili
Januari 22, 2023, Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga kwa kushirikiana
na wadau wengine wa Sheria, imezindua maadhimisho ya wiki ya sheria nchini, katika
uwanja wa Zimamoto ambako elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria
itaendelea kutolewa mpaka siku ya kilele tarehe Februari 1, Mwaka huu 2023.
Hafla hiyo pia imehudhuriwa na wadau, wananchi pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali akiwemo Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mh: Elias Ramadhan Masumbuko.
Kaulimbiu ya
maadhimisho ya wiki ya sheria kwa mwaka huu inasema kuwa “utatuzi wa migogoro katika usuluhishi
kwa ajili ya kukuza uchumi endelevu”
Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Joseph Mkude akizungumza kwa niamba ya mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kwenye uzinduzi wa wiki ya kisheria yanayofanyika kwenye uwanja wa Zimamoto Nguzonane mjini Shinyanga.
Jaji Mfawidhi wa Mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Shinyanga Athumani Matuma akizungumza kwenye uzinduzi wa wiki ya kisheria yanayofanyika katika uwanja wa zimamoto Nguzonane mjini Shinyanga.
TAZAMA PICHA ZOTE HAPA CHINI
Post a Comment