Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria
imeikumbusha serikali kupitia Halmashauri zake kuhakikisha inaendeleza miradi yote
inayoanzishwa na wananchi ili kuleta
tija zaidi katika jamii.
Akizungumza baada ya kamati hiyo kutembelea na kukagua miradi mbalimbali
ya maendeleo katika Manispaa ya Shinyanga, Makamu Mwenyekiti wa
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria (Mb)Florent Kyombo amesema
ni muhimu miradi inayoanzishwa na wananchi kuendelezwa ili kuleta matokeo
chanya kwa uharaka.
Mhe. Kyombo amesisitiza kuwa serikali kupitia
Halmashauri zake ni vyema kujenga tamaduni za kuendeleza na kuboresha miradi
inayoanzishwa na wananchi ili iweze
kuleta manufaa Zaidi ikiwemo miradi inayotekelezwa na walengwa wa
kaya maskini kupitia mfuko wa maendeleo
ya jamii TASAF.
---INSERTS…KYOMBO---
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala, Katiba na Sheria (Mb)Florent Kyombo amewaomba wananchi wa Mkoa wa
Shinyanga kuendelea kushirikiana na serikali katika utekelezaji wa miradi ya
maendeleo ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
Kwa upande wao baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu
ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria akiwemo Mbunge wa jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace
Butondo wamewaasa wanufaika wa miradi ya TASAF kutumia vizuri fedha wanazopata
katika utekelezaji wa miradi hiyo na kwamba waepuke matumizi mabaya ya fedha
ikiwemo ulevi na mambo mengine yasiyofaa kwenye familia na jamii kwa ujumla.
Wajumbe wa kamati hiyo pia wameiomba serikali
kushughulikia changamoto zinazowakabili walengwa wa kaya maskini ikiwemo changamoto
ya upatikanaji wa namba za NIDA ambayo ni changamoto kubwa katika jamii.
Akizungumza Waziri wa
Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Jenista Mhagama amesema katika utekelezaji wa miradi ya TASAF serikali imetenga
fedha kiasi cha shilingi Bilioni 496 ambapo Bilioni 51.014 zitawanufaisha
wakazi wa Mkoa wa Shinyanga.
Waziri Mhe. Mhagama amewasisitiza
viongozi wa Halmashauri wanaosimamia fedha hizo kuhakikisha zinatumia vizuri
ili kufikia malengo yaliyokusudiwa na serikali.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi Christine Mndeme amemshukuru
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta
fedha za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo sekta ya elimu,
afya, pamoja na miundombinu.
Amesema Mkoa wa Shinyanga wananchi 44,252 wanaendelea
kunufaika na mpango wa TASAF ambapo jumla ya miradi 598 inayosimamiwa na mpango
wa TASAF Mkoa wa Shinyanga inaendelea vizuri.
RC Mndeme ameihakikishia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya
Utawala na Katiba na Sheria kuwa Mkoa wa Shinyanga utaendelea kuibua na
kuiendeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kushirikiana na jamii husika.
Aidha Mndeme amesema ataendelea kusimamia matumizi
sahihi ya fedha za miradi mbalimbali ya maendeleo ili kuwasaidia wananchi
kuinuka kiuchumi katika maisha yao ya kila siku.
Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga Mhe. Elias
Radhaman Masumbuko amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.
Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za maendeleo katika Manispaa hiyo ambapo ameahidi
kuendelea kushughulikia changamoto zinazowakabili wananchi ili kuendana na kasi
ya mabadiliko ya kimaendeleo.
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria
pamoja na mambo mengine imetembelea na kukaguzi ujenzi wa jengo la Ofisi ya
Taifa ya Mashtaka Mkoa wa Shinyanga ambalo linaendelea kujengwa kwa lengo la
kusogeza karibu huduma za kimashtaka karibu na wananchi.
Akitoa taarifa za ujenzi wa jengo hilo kwa kamati
hiyo, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Pauline Gekul amesema kuwa septemba 26
mwaka 2022 Ofisi ya Taifa ya Mashtaka iliingia Mkataba na Mkandarasi Eliroi
Construction kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mashtaka Mkoa wa
Shinyanga wenye thamani ya Bilioni 2.15 ikijumuisha ongezeko la Thamani VAT.
Gekul amesema kuwa mradi huo una Taraji kukamilika
ndani ya muda wa miezi 8 ambapo ulianza kuteklelezwa November 22,2022 ambapo
unataraji kukamilika June 22 ambapo mpaka sasa umefikia asilimia 35.
Bi Gekul ameongeza kwa kusema kuwa mpaka sasa
mkandarasi amekwisha lipwa fedha za awali kiasi cha shilingi milioni 323 kati
ya bilioni 2.15 huku Mkandarasi Mshauri Mwelekezi wa mradi Water Institute
kawazulite maombi ya kulipwa kiasi cha shilingi milioni 335.5
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester
Mwakitalu ameishukuru Kamati hiyo kwa juhudi zake kubwa za kuipigania Ofisi
hiyo ambapo kwa mwaka huu wa fedha unaondelea jumla ya mikoa sita imepatiwa
fedha za ujenzi wa Ofisi ikiwa ni pamoja na Shinyanga,Geita,Manyara, Rukwa,
Katavi na Njombe na kufanya idadi ya ofisi zinazojengwa kufikia kumi.
DPP Mwakitalu ameushukuru uongozi wa Mkoa wa Shinyanga
chini ya Mkuu wa Mkoa huo Christine Mndeme kwa kuwapatia eneo la Kiwanja kwa
ajili ya ujenzi wa Ofisi hiyo ambayo itasaidia na kurahisisha utoaji wa huduma
kwa jamii juu ya masuala ya Mashtaka ambapo amesema eneo hilo awali ilipewa
taasisi nyingine.
DPP Mwakitalu amesema kuwa ujenzi huo utakapokamilika
utarahisisha utaoaji wa huduma kwa jamii ambapo watumishi watakuwa na sehemu
bora na mazingira rafiki ya utaoji wa huduma kwa wananchi.
Mkandarasi anayetekeleza ujenzi wa mradi huo kampuni
ya Eliroi Construction Bw Ngakuka Ngakuka amesema kuwa mradi huo umechelewa
kufikia asilimia 50 mpaka sasa kutokana na kuchelewa kwa malipo ya awali
sambamba hilo Ngakuka amesema kuwa licha ya kuraisi cheti cha malipo yanakwama
kutoka kwa wakati
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Katiba na
Sheria imefanya ziara ya kukagua na kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa
na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza Waziri wa
Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Jenista Mhagama wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria Wakiwa katika ukaguzi wa Barabara
ambayo imetengenezwa na Walengwa wa TASAF Mtaa wa Mwadui Kata ya Ngokolo
Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza Waziri wa
Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.
Jenista Mhagama wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na
Sheria Wakiwa katika ukaguzi wa Barabara
ambayo imetengenezwa na Walengwa wa TASAF Mtaa wa Mwadui Kata ya Ngokolo
Manispaa ya Shinyanga.
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza katika hafla hiyo
Naibu Waziri wa Nchi Ofisi
ya Rais Menejimenti ya utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Ridhiwani
Kikwete akizungumza katika hafla hiyo
Post a Comment