" ACT WAZALENDO MKOA WA SHINYANGA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA ZITO KABWE MGENI RASMI

ACT WAZALENDO MKOA WA SHINYANGA KUFANYA MKUTANO WA HADHARA ZITO KABWE MGENI RASMI

Na Mapuli Misalaba, Shinyanga

Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Mkoa wa Shinyanga Bi Siri Yassin  amesema chama hicho kinatarajia  kufanya Mkutano wa hadhara Mei 11, Mwaka huu 2023 Mjini Shinyanga.

Akizungumza na Misalaba Blog Mwenyekiti huyo amesema Mkutano huo utafanyika katika uwanja wa zimamoto eneo la Nguzonane kata ya Kambarage Mjini Shinyanga.

Amesema viongozi wanaotarajiwa kuhudhuria ni pamoja na Mwenyekiti wa chama hicho Taifa Bwana Zito Kabwe ambapo amewaomba wanachama pamoja na wananchi wengine wa Mkoa wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi kuhudhuria mkutano huo.

Bi. Siri Yasin amesema kabla ya Mkutano huo viongozi pamoja na wanachama wa chama hicho watashiriki shughuli za kijamii ikiwemo kupanda miti,na kuchangia damu salama.

Post a Comment

Previous Post Next Post