" DKT. BATILDA: NITAKUWA WA KWANZA KUWACHARAZA VIBOKO WALIMU WATAKAOBAINIKA KUFANYA UKATILI KWA WANAFUNZI.

DKT. BATILDA: NITAKUWA WA KWANZA KUWACHARAZA VIBOKO WALIMU WATAKAOBAINIKA KUFANYA UKATILI KWA WANAFUNZI.

Na Lubango Mleka - Misalaba Blog, Igunga.

 MKUU wa Mkoa wa Tabora Dkt. Batilda Burian amewaonya Walimu ambao watabainika kuwafanyia ukatili Wanafunzi ikiwa ni pamoja na kufanya mapenzi na Wanafunzi wakike, kuwalawiti wanafunzi wa kiume na hata kwa Walimu wa kike ambao watabainika kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja (usagaji).   

 Hayo ameyabinisha alipokuwa anazindua miradi ya maji inayosimamiwa na Mamlaka ya Maji Mjini na Vijijini Wilaya ya Igunga (RUWASA) ambayo yameendana sambamba na kilele cha maadhimisho ya miaka 59 ya Muungano wa Tanzania.

 “Nipende kuongea na wanafunzi na walimu ambao leo mmekuja hapa katika uzinduzi huu wa miradi ya maji, hivi karibuni kumeibuka janga kubwa katika nchi yetu la ushoga na usagaji, watoto wetu wa kiume wamekuwa wakiingiliwa kinyume na maumbile na walimu na wengine kubakwa, hivyo niwaombe wanafunzi wote ukiona mwalimu anakushikashika katika sehemu za makalio kwa watoto wa kiume na kwa wakike pia toa taarifa kwa walimu wengine au mwambie mzazi wako na hata viongozi wa vijiji,” alisema Dkt Balozi Buriani.

 Aliendelea kusema kuwa, “Endapo mtu huyo anayekufanyia ukatili akakutishia eti ntakuuwa au ukitoa siri utaona usisite kutoa taarifa sawa, na endapo ikabainika kuwa mwalimu umefanya jambo hili nitakuwa wa kwanza kumchapa viboko kabla hajafikishwa Polisi na kama mzazi nitaita makamanda watamcharaza viboko, jambo hili linasikitisha sana nanyinyi wananchi wa Imalililo msikubali jambo hili likatoke kwa watoto wenu au vijana wenu, toeni taarifa kwa mtu mtakaye mbaini kufanya uovu huo.”

 Aidha, Dkt Batilda, ameipongeza RUWASA wilaya ya Igunga kwa kuendelea kusimamia vyema miradi ambayo wanaitekeleza, jambo ambalo limeendelea kupunguza kero kwa wananchi wa vijijini kwa kukosa huduma ya maji safi na salama kwa miaka mingi.

 Kwa upande wake meneja wa RUWASA Igunga Mhadisi Marwa Sebastian Muraza, akisoma taarifa ya miradi hiyo, amemshukuru Rais Dkt Samia Hassan Suluhu kwa kuendelea kuipatia fedha za utekelezaji wa mairadi RUWASA na kuahidi kuendelea kusimamia miradi hiyo kwa ubora zaidi na kwa wakati ili kutatua changamoto ya ukosekanaji wa maji safi na salama kwa wananchi wa vijijini, jambo ambalo litawaondolea magonjwa ya mlipoko kama vile homa ya matumbo, kuhara damu, magonjwa ya ngozi na kipindupindu pamoja na hatari ya kujeruhiwa na wanyama wakali kama vile fisi na tembo.

 “Ndugu mgeni rasmi tunaomba utuzindulie hii leo miradi yetu ya maji katika vijiji vya Imalilo, Matinje utanufausha wananchi 1,613, Kinungu watanufaika jumla ya wananchi 4,554, Mangungu jumla ya wanufaika 2,797, Mibuyumiwili na Itunduru wananchi ni 7,074 wamefikiwa na huduma ya maji, Ntigu na kijiji cha Moyofuke ni jumla ya wanakijiji 40,013, kwa vijiji vya Ziba na Igumila  ni wananchi 4,846 watanufaika na maji haya." alisema Mhandisi Muraza.

 Alimalizia kwa kusema kuwa "mwisho ni kijiji cha Buchenjegele na Matindje ambapo wananchi wa vijiji hi ni 7,054 watanufaika, miradi hii yote imekamilika kwa asilimia 100 na itasimamiwa na jumuiya ya watumiamji  (CBWSO) chini ya usimamizi wa wataalamu kutoka RUWASA Igunga na tayari wananchi na jumuiya wameisha panga bei za uuzaji maji haya kwa ndoo itagharim shilingi 100, miradi yote hii imegharimu kiasi cha shilingi 2,347,690,023."

 Nao baadhi ya madiwani wa kata zilizozinduliwa miradi hii ya maji kwa jimbo la Manonga na Igunga mjini waliojitamburisha kwa majina ya Joladi Milenge  kata ya Kinungu, Hyasinta Ngassa kata ya Nguru kwa niaba ya madiwani wenzao wamemshukuru Rais Dkt Samia, Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt Balozi Batilda Buriani, Mkuu wa wilaya ya Igunga Sauda Mtondoo, watumishi wote wa RUWASA mkoa wakiongozwa na Mhandisi Hatari Kapufi, wabunge wa jimbo la Manonga na  Igunga mjini pamoja na viongozi wote wa vijiji kwa kusimamia na kuitekeleza Ilani ya CCM kwa kusimamia miradi hii vyema.

 Huku baadhi ya wananchi waliojitambulisha kwa majina ya Jane Luhenda, Grace Elias,Habiba Hamis, Bernadeta Shija na Stephan Jelemia wamepongeza serikali kwa kuwakumbuka na kuwafikishia maji safi na salama kwani vijiji vyao tokea nchi ya Tanzania imepata uhuru hawa kuwa na huduma ya maji safi na salama.

 “ Nimefurahi sana leo kupata maji kwani wanafunzi wetu walikuwa watolo shuleni kwa kufuata maji mabili mwanafunzi anaondika saa moja asubu kufuata maji anarudu saa tisa macha hivyo kumfanya kukosa masomo, hata ndoa zetu sasa zitakwenda kuimarika na kumaliza kabisa ukatili wa vipogo kwa wanawake na mabinti kubakwa na hata saazingine watoto wa kiume kulawitiwa hivyo sasa matukio haya yanakwenda kuisha hapa kijijini kwetu,” alisema Jane Luhende.


Post a Comment

Previous Post Next Post