Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Serikali
Wilayani Shinyanga imewakumbusha wazazi na walezi kuwajibikia jukumu la malezi
na makuzi bora kwa watoto ili kuandaa taifa lenye kizazi chenye maadili mema.
Kauli
hiyo imetolewa na katibu tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi
kwenye hafla iliyowakutanisha
wazazi,walezi na watoto wanaoishi katika
mazingira magumu kwenye mitaa mbalimbali
Mjini Shinyanga,ambayo imeandaliwa na shirika lisilo la kiserikali Nancy Foundation kwa kushirikiana na serikali.
Katibu
tawala huyo amesisitiza wazazi na walezi kusimamia na kufuatilia mienendo ya
watoto ili kudhibiti wasijihusishe na makundi yasiyofaa,ikiwa ni pamoja na
kuwapatia mahitaji yote ya msingi
ikiwemo haki elimu.
“Ukimlea vizuri mtoto wako ipo siku atakuja kuwa wa
msaada sana kwako kwahiyo wewe muombe mwenyezi Mungu jikusanye kusanye kwa
chochote unachoweza kupata ili hatimaye mtoto umfikishe kwenye hatua furani
sisi akina mama lazima tuone uchungu na tuone haja ya kuwalea watoto wetu”
“Lakini serikali haiwezi kuwaacha akina Baba waendelee
kukataa watoto kuna namna ya kumshurutisha atoe matunzo kwa mtoto kwahiyo mama
hakikisha unatoa taarifa kuna madawati ya njinsia ili serikali iweze kumchukulia
hatua”.amesema Bwana Chambi
Mkurugenzi
wa Shirika la Nancy Foundation Bwana Erza Manjerenga ameeleza hatua mbalimbali
zilizofikiwa na mradi huo ambao umelenga kuwaokoa watoto wanaoishi na kufanya
kazi mitaani katika Manispaa ya Shinyanga.
“Leo tulikuwa na kikao cha wazazi peke yao kuweza
kujua sasa wao wanasema nini kuhusu changamoto zilizobainishwa na watoto wao
lakini nao wazazi wamezungumza changamoto zao ikiwemo kukosa ada za wanafunzi,
ugumu wa maisha na changamoto zingine hatua inayofuata ni kuhakikisha
tunazifanyia kazi hizi changamoto zao zote tayari tumehakikisha kuwaunga na
bima ya afya ambayo inatolewa na serikali CHF iliyoboreshwa ili wazazi hawa
wawe salama wakazi wa magonjwa, maradhi katika familia yao lakini kingine ni
kuona namna ya kusaidia kama vifaa vya shule”.
“Changamoto tuliyokutana nayo ni wazazi kushiriki wa
kike wazazi wa kiume hakuna hata mmoja tunatamani sana kuona wazazi wa jinsia
zate mwanaume na mwanamke wanashiriki pamoja ili tuweze kutatua changamoto hizi
kwa uharaka watoto watimize ndoto zao”.amesema
Mkurugenzi Manjerenga
Baadhi
ya wazazi na walezi wa watoto wanaoishi mitaani wameahidi kushirikiana na
shirika hilo pamoja na serikali katika
juhudi za kuwaondoa watoto hao kwenye mazingira hatarishi ya mitaani.
Mashirika
mawili yasiyokuwa ya kiserikali Mkoani Shinyanga Nancy Foundation na Ubongo
learing yanatekeleza mradi wa kupunguza au
kumaliza tatizo la watoto wanaoishi na kufanya kazi mtaani, mradi huo
unaoitwa “Home is where the heart is” .
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi akitoa elimu kwa baadhi ya
watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani katika Manispaa ya Shinyanga.
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi akitoa elimu kwa baadhi ya
watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani katika Manispaa ya Shinyanga.
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi akiwa katika kikao cha
pamoja na wazazi na viongozi mbalimbali wa serikali.
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi akiwa katika kikao cha
pamoja na wazazi na wawatoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani kilichoandaliwa
na shirika la Nancy Foundation
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi akisisitiza mambo
mbalimbali ya muhimu kwa wazazi wa watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi akisisitiza mambo
mbalimbali ya muhimu kwa wazazi wa watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.
Zoezi
la watoto wenye nywele ndefu kunyolewa likiendelea katika ukumbi wa Mazingira
Center Manispaa ya Shinyanga.
Mwezeshaji
kutoa polisi dawati la jinsia ambaye pia ni polisi wa kata ya Mjini Shinyanga
ALINSP Jane Mwazembe akiendelea na zoezi la kuwapa chakula watoto wanaoishi na
kufanya kazi mitaani katika Manispaa ya Shinyanga.
Afisa
ustawi wa jamii wa Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga Lemiflora Nyalaja
akiendelea na zoezi la kuwapa maji ya kunywa watoto wanaoishi na kufanya kazi
mitaani.
Katibu
tawala wa wilaya ya Shinyanga Bwana Boniphace Chambi upande wa kushoto,
Mwenyekiti wa mtaa wa Miti mirefu Bwana Nassor Warioba katikati na Mkurugenzi
wa Shirika la Nancy Foundation Bwana Erza Manjerenga upande wa kulia wakiwa
katika mazungumzo ya pamoja
Post a Comment