" AJALI YAUA MMOJA NAMAJERUHI BUGWETO MANISPAA YA SHINYANGA

AJALI YAUA MMOJA NAMAJERUHI BUGWETO MANISPAA YA SHINYANGA

 

Mtu Mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Daud kulwa Mwandu Mwenye

umri wa Miaka 25,Mkazi wa Bugweto kata ya Chamaguha amefariki

Dunia baada ya kugongwa na Gari kwenye Barabara kuu ya Shinyanga

Mwanza.

Kwa mujibu wa watu walioshuhudia tukio hilo, ajali hiyo imetokea

majira ya saa Nne asubuhi Daud akiwa amebebwa kwenye usafiri wa

Baiskeli ndipo Gari hiyo ilipowagonga na kusababisha kifo chake papo

hapo.

Wameeleza kuwa mwendesha baiskel Athuman Mtatiro mwenye umri

wa miaka 33,mkazi wa tambukareli aliyekuwa amempakiza Daud

ambaye kwa sasa ni marehemu amekimbizwa hospitali ya Manispaa ya

Shinyanga kwa ajili ya matibabu

Kufuatia ajali hiyo wakazi wa maeneo hayo wamelalamikia madereva

kuendesha mwendo kasi hali inayochangia ajali za mara kwa mara

ambazo zimekuwa zikisababisha vifo na majeruhi.


Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Manispaa ya Shinyanga Dkt PIELINA

MWALUKO amethibitisha kupokea Mwili wa Marehemu huyo na

majeruhi mmoja ambaye amelazwa kwa ajili ya matibabu.


Kwa upande wake kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga

kamishina msaidizi wa Polisi Janeth Magomi amelitaja gari hilo kuwa ni

aina Toyota Landcruser T.652 DST iliyokuwa ikitokea Mjini kuelekea

maeneo ya Ibadakuli ikiendeshwa na Sheikh Ismail Habib Makusanya.

Post a Comment

Previous Post Next Post