" SASA HIVI HUWEZI KUFANYA JAMBO LOLOTE BILA KUWA NA KITAMBULISHO CHA NIDA – DC MKUDE

SASA HIVI HUWEZI KUFANYA JAMBO LOLOTE BILA KUWA NA KITAMBULISHO CHA NIDA – DC MKUDE

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude amewataka wakazi wa wa Wilaya hiyo kujitokeza kwa wingi kuchukua vitambulisho vya Uraia (NIDA).

Amesema vipo vikundi pamoja na baadhi ya wananchi wamekuwa wakikosa fursa mbalimbali ikiwemo mikopo kwa sababu ya kutokuwa na kitambulisho cha Uraia (NIDA).

DC Mkude amehimiza wakazi wa Wilaya ya Kishapu kujitokeza kwa wingi  kwenda kuchukua vitambulisho hivyo ili viweze kuwasaidia katika fursa mbalimbali zinazojitokeza.

Amesema vitambulisho vya Uraia (NIDA) 67864 vimesambazwa kwenye ofisi za watendaji wa kata katika Wilaya ya Kishapu ambapo amesisitiza wananchi kwenda kuchukua vitambulisho vyao.

“Vitambulisho hivi tumekuwa tukivisubiri kwa muda mrefu lakini sasa hivi tunaenda kwenye matumizi makubwa ya vitambulisho hivi huwezi kufanya jambo lolote bila kuwa na kitambulisho cha NIDA, sasa hivi hata mikopo wanasisitizwa kuwa na vitambulisho hivi ili kupata mkopo sasa niwaombe wananchi wajitokeze kwenda kuchukua vitambulishi vyao kwenye ofisi za watendaji wa kata”amesema DC Mkude

Baadhi ya wakazi wa Wilaya hiyo ya Kishapu Mkoani Shinyanga wamesema vitambulisho hivyo vitasaidia kwa kiasi kikubwa kufanikisha mambo mbalimbali yanayojitokeza kama fursa kwa vikundi na mtu mmoja mmoja.Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude (Kulia) akimkabidhi boksi la vitambulisho vya Uraia (NIDA), msajiri wa Wilaya ya Kishapu Bwana Fred Mwasipu.

 

Post a Comment

Previous Post Next Post