Baadhi ya wakazi wa Manispaa ya Shinyanga wamemwomba Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Mhe. Anamringi Macha kushughulikia Changamoto zilizopo ikiwemo
uboreshaji wa miundombinu ya Barabara
wakiitaja Barabara kipande cha kutoka Ndala, kupitia Masekelo kwenda Mwawaza ilipo Hospitali ya rufaa ya
Mkoa wa Shinyanga.
Wananchi hao wamemwomba Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga kuendelea kutatua kero na changamoto za muda
mrefu ikiwemo kuiboresha Barabara hiyo ya kuelekea Hospitali ya rufaa ya Mkoa
wa Shinyanga.
Wametoa maoni hayo wakati wakizungumza na Misalaba Media ikiwa ni siku
mbili baada ya Mkuu Mpya wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha kukabidhiwa
ofisi siku chache baada ya kuapishwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kufuatia
uteuzi wake uliofanyika March 12,Mwaka huu
Wameshauri pia kuwa itapendeza iwapo Mkuu wa Mkoa atajenga utaratibu wa
kusikiliza kero za Wananchi kupitia Mikutano ya hadhara ili kufahamu changamoto
zinazowakabili.


Post a Comment