Na Mapuli Kitina
Misalaba
Askofu Mkuu wa kanisa
la AICT Tanzania na Askofu wa Dayosisi ya Mwanza Mussa Magwesela amewataka
Wazazi na Walezi kuwa chachu ya kukuza na kuendeleza karama za watoto katika
maisha ya kanisa.
Ameyasema hayo leo
wakati akihubiri kwenye ibada ya Jumapili katika kanisa la AICT Kambarage mjini
Shinyanga, ambapo amesema kanisa linatambua na kuthamini karama
za watoto hivyo kwa kushirikiana na wazazi na walezi, litaendelea kuibua uwezo wao na kuwaendeleza kupitia
vipaji vyao.
Amesema hatua hiyo
itasaidia kutimiza ndoto za watoto na kuendelea kulitumikia taifa katika
misingi ya Dini.
Post a Comment