Na Moshi Ndugulile
Mtoto Mmoja mwenye umri
wa Miaka Mitano Shamimu Tumaini Jumaissa mkazi wa kijiji cha Ibanza kata ya
Mwamala Wilaya ya Shinyanga ameuawa kwa kushambuliwa na fisi wakati akiokota
kuni jirani na nyumbani kwao.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti
wa kijiji cha Ibanza Bwana Hassan Issa
Barabara amesema tukio hilo limetokea jana majira ya Saa kumi na mbili jioni
wakati Mtoto huyo akiwa na mwenzake wakiokota kuni hatua chache kutoka nyumbani
kwao, ndipo fisi huyo alipomvamia na
kumburuza Mtoto huyo na kisha kukimbia naye vichakani.
Amesema baada ya kutokea
tukio hilo wanakijiji walianza kufuatilia michirizi ya damu na ndipo walipomkuta
Mtoto huyo akiwa amepoteza maisha huku akiwa ameshambuliwa vibaya sehemu za uso
na kichwani.
“Watoto
hao wawili walikuwa wanaokota kuni kwenye muda wa saa kumi na mbili inaelekea saa
moja ghafla akatokea Fisi kale katoto kana umri wa Miaka mitano harakati za
kukimbia Yule mwenzake anaumri wa Miaka Tisa yeye alifanikiwa kukimbia na
bahati nzuri kulikuwa na Mama jirani akakasikia kale katoto kanalia kuangalia
akamuona Fisi amemny’ata sasa huyo mama akaanza kupiga kelele Fisi nayeye akawa
anatokomea”.
“Baada
ya hapo watu sasa tukajitokeza baada ya kusikia kelele usiku uliingia Fisi Yule
alitokomea na mtoto tukaanza juhudi za kumsaka huku wasalama wanapiga penga tukakusanyikana
kwenye tukio tukaendelea kusaka muda kama wa masaa matatu haonekani baadaye
tukarudi sehemu ya tukio tukaanza tena kufuatilia damu mpaka alipo tukamkuta na
Fisi anaendelea kumla huyo mtoto lakini Fisi alikimbia baada ya kutuona ikabidi
tu tumchukue mtoto kumrudisha Nyumbani”.amesema Mwenyekiti
Hassan
Misalaba Media
imezungumza na Felista Elias Mkazi wa kijiji cha Ibanza ambaye ameshuhudia tukio hilo na hapa
ameeleza kuwa hakupata msaada wa haraka kumwokoa mtoto huyo kwa kuwa
wakati huo wanaume wa kijiji hicho walikuwa mbali kwenye shughuli za Sungusungu.
“Mtoto
aliyefanyiwa hilo tukio mimi ni jirani yao niliwaona wanaokota kuni baadaye
walipeleka hizo kuni baada ya hapo wakaenda kurudi tena, waliporudi mara ya
pili kidogo tu dakika kama moja hivi nikasikia wameanza kulia walikuwa wawili
ndiyo nikasogea barabarani kuwauliza mnalilia nini sasa kale katoto kakubwa
kakawa hakanisemeshi kanakimbia tu baada ya kukasikia kale kengine kanalia ndiyo
nikageuka kuangalia nikaona Fisi amekabeba akawa anakaburuza mimi nilishindwa
namna ya kufanya nikaanza kupiga tu kelele kwa bahati mbaya wanaume wote
hawakuwepo ilikuwa imegongwa kengele ya Sungusungu walijitokeza tu wanawake ila
badaye watu wakawa wengi na wanaume walikuja”.amesema
Felista Elias
Afisa Mtendaji wa
kijiji cha Ibanza Bi. Tausi Kabadi amesema baada ya tukio hilo kutokea serikali
ya kijiji imetoa taarifa kwa jeshi la polisi na kisha kuwasiliana na maafisa wa
wanyamapoli na Maliasili na kwamba kwa hatua za awali Sungu sungu wameanza
kumsaka mnyama huyo.
Post a Comment