" DARAJA LA UPINDE WA MAWE KURAHISISHA MAWASILIANO KWA WANANCHI MKOANI KILIMANJARO

DARAJA LA UPINDE WA MAWE KURAHISISHA MAWASILIANO KWA WANANCHI MKOANI KILIMANJARO

Na Mary Mosha, SIHA


BAADHI  ya wananchi  wa kijiji cha Munge wilayani Siha, Mkoani Kilimanjaro wamesema upatikanaji wa daraja la Upinde wa Mawe  litawarahishia  mawasiliano  katika kijiji  na kijiji,  kupunguza utoro shuleni  pamoja na kupata  mahitaji ya msingi  kwa urahisi.


Wakizungumza mara baada ya mwenge wa uhuru kuweka jiwe la msingi   akiwemo   Florah Letaiyo alisema,  awali nyakati za mvua walikuwa wakilala njaa  kutokana na kukosekana kwa mawasiliano katika eneo hilo.


"Wanafunzi wengi hukosa shule sikumbili hadi sita hasa nyakati za mvua.kama hujanunua mahitaji au kusaga unga mvua zinaponyesha ni ngumu kupata maana upande wa juu ndiko zinakopatikana na hutenganishwa na daraja,"alisema  Julieth  Molel 


Baadhi ya madereva akiwemo  Abel Saruni alisema   kukamilika kwa daraja hilo kunaweza  kukuza Uchumi  wa madereva bodaboda, na jamii kwa ujumla.


Naye Diwani  wa viti maalumu wa   Kata Donyomoro, Lillian John   alisema  kabla ya daraja hilo wapo baadhi walishasombwa na maji  wakielekea kwenye utafutaji wa majukumu.


"Kulikuwa na utoro mwingi shuleni hasa  nyakati za mvua  hivyo kuwafanya baadhi ya wazazi hasa ya jamii ya wafugali kukata taama,"alisema 


Akisoma  taarifa   Mtendaji  wa kijiji hicho, Winner Muro  alisema mradi huo  unatarajiwa kugharimu zaidi ya milion 35 zikiwemo fedha za mapato ya ndani ya halimashauri zaidi ya milion 27  wafadhili(TASAF)zaidi ya milion 540 na michango ya jamii zaidi ya milion 7 na kutoa ajira  wananchi 13.


Aidha akiweka jiwe la msingi, kiongozi wa mbio za mwenge 2024, Godfrey Mzava  aliitaka viongozi wa halmashauri  kuhakikisha wanafanya mawasiliano  na wananchi waliopo pembezoni mwa  hifadhi ya barabara na kuona namna ya kuwafidia au kupisha ili kuepuka madhara yatokanayo na  kuishi pembezoni mwa barabara lilipo daraja hilo.


"Mradi tumeukaugua na kuutembelea, umekamilika kwa asilimia 96 na hii ndogo iliyobaki ni vitu vidogo vidogo, vikamilishwe.Wananchi  ni wajibu wenu kuwa walinzi wa miradi hii ili thamani  ya fedha ya serikali kuleta tija kwa jamii, "alisema Mzava. 





Post a Comment

Previous Post Next Post