" DIWANI ZAMDA SHABAN ATOA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM NDALA, ZAIDI YA MILIONI 276 ZATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

DIWANI ZAMDA SHABAN ATOA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM NDALA, ZAIDI YA MILIONI 276 ZATEKELEZA MIRADI YA MAENDELEO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, ameendesha mkutano wa hadhara kwa ajili ya kuwashukuru wananchi kwa ushirikiano waliompa tangu achaguliwe mwaka 2020, huku akitoa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa kipindi cha miaka minne iliyopita kuelekea mwisho wa kipindi chake cha miaka mitano.

Katika taarifa hiyo, Mhe. Zamda amesema kata ya Ndala imepiga hatua kubwa katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, miundombinu, afya, TEHAMA, umeme, mikopo kwa vikundi, na upimaji wa ardhi, akiahidi kwamba kwa siku chache zilizobaki, hatamaliza muda wake bila kukamilisha changamoto zilizobaki.

Amesema kuanzia mwaka 2021 hadi Februari 2025, idadi ya wanafunzi katika shule ya Msingi Msufini na Ndala Sekondari imeongezeka kwa asilimia 100 kutokana na utekelezaji wa Mpango wa Elimu Bila Malipo. Aidha, ufaulu kwa wanafunzi wa Ndala Sekondari umeongezeka kutoka 97% mwaka 2023 hadi 98% mwaka 2024, hatua iliyofanikisha shule hiyo kupokea wanafunzi wengi na kushika nafasi ya juu katika Manispaa.

Zaidi ya shilingi milioni 276 zimetumika katika miradi mbalimbali ya elimu kama ifuatavyo:

Ndala Sekondari

  • Maabara ya Sayansi (2021) – Tsh 30 milioni
  • Ukamilishaji darasa (nguvu za wananchi) – Tsh 5.42 milioni
  • Vyoo 12 – Tsh 13.2 milioni
  • Vyumba 2 + ofisi na samani (2022) – Tsh 40 milioni
  • Vyumba 4 + samani (2023) – Tsh 80 milioni

Shule ya Msingi Msufini

  • Darasa (nguvu za wananchi) – Tsh 15 milioni
  • Vyumba 3 + samani (2023) – Tsh 78 milioni
  • Vyoo 3 – Tsh 6.6 milioni

Shule ya Shikizi Msufini B

  • Vyumba 2 + ofisi (hatua ya lenta, nguvu za wananchi na mfuko wa jimbo) – Tsh 9.3 milioni

Zamda ameeleza kuwa kata ya Ndala  imenufaika na miradi mingi ya barabara kwa kipindi cha miaka minne. Hadi sasa, barabara kadhaa zimetengenezwa kwa kuchongwa, kujengwa mitaro na makalavati katika mitaa ya Banduka, Mwabundu, Mlepa, Ndala, Mapinduzi na maeneo mengine, ikiwa ni pamoja na:

  • Ujenzi wa daraja la Ndala – Mwasele: Tsh 103.2 milioni
  • Ujenzi wa mitaro na makalavati mbalimbali: Zaidi ya Tsh 80 milioni

Amesema kupitia mpango wa mikopo ya Halmashauri, kikundi cha watu wenye ulemavu kiitwacho I CAN kilipatiwa mkopo wa Tsh milioni 20 kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi.

Diwani huyo ameeleza kuwa mtaa wa Mlepa tayari umeunganishwa na umeme, huku mtaa wa Ndala upo kwenye hatua za kusimikwa kwa nguzo na kufungwa nyaya.

Zaidi ya viwanja 3,262 vimepimwa kwenye mitaa mbalimbali:

  • Mlepa: Viwanja 1,050
  • Mwabundu: Viwanja 1,212
  • Ndala: Zoezi la kupima na kugawa namba linaendelea

Kata hiyo haikuwa na kituo cha afya tangu 2020, lakini mwezi Januari 2025 eneo limepatikana na wamiliki wote wamelipwa fidia. Ujenzi wa kituo cha afya unatarajiwa kuanza mwaka 2026.

Kata ya Ndala sasa ina watendaji katika kila mtaa isipokuwa mmoja ambao nao unatarajia kupata mtendaji muda wowote. Idara ya elimu pia imeongezewa walimu, hali iliyoboreshwa zaidi na ajira za serikali zinazoendelea.

Katika hatua nyingine, Kata ya Ndala imefungua soko la kisasa lililowekewa mageti kwa Tsh milioni 5. Pia, gulio jipya limeanzishwa linalofanyika kila Jumatano, likihudumia wakazi wa Ndala na maeneo jirani.

Amesema shule ya Sekondari Ndala imepata kompyuta 2 na printa kwa ajili ya elimu ya TEHAMA. Ofisi ya kata nayo imenunua kompyuta moja ambayo imerahisisha utoaji wa huduma na uandaaji wa taarifa.

Wakizungumza baada ya mkutano huo, baadhi ya wananchi wa Ndala wamepongeza kazi kubwa ya maendeleo iliyofanyika, huku wakimuomba Mhe. Zamda kuhakikisha changamoto zilizobaki zinamalizwa kwa wakati.

Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara.

Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara.

Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, akiwashukuru wananchi.

 Afisa Elimu wa kata ya Ndala Mwalimu Imani Chambulilo akizungumza kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo.Afisa Elimu wa kata ya Ndala Mwalimu Imani Chambulilo akizungumza kwenye mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa na Diwani wa kata hiyo.


Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara.

Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara.

Diwani wa Kata ya Ndala ambaye pia ni Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga, Mhe. Zamda Shaban, akizungumza kwenye mkutano wake wa hadhara.

Post a Comment

Previous Post Next Post