" DR. SAMIA - KATAMBI DAY YAZAA NEEMA KWA WANANCHI WA SHINYANGA KATAMBI ATOA MAMILIONI KILA KATA KUCHOCHEA MAENDELEO

DR. SAMIA - KATAMBI DAY YAZAA NEEMA KWA WANANCHI WA SHINYANGA KATAMBI ATOA MAMILIONI KILA KATA KUCHOCHEA MAENDELEO

Na Mapuli Kitina Misalaba

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Paschal Katambi, amesema Serikali imejipanga kutatua changamoto za miundombinu ya barabara katika Manispaa ya Shinyanga, na kwamba kazi hiyo itafanyika kwa viwango vya kisasa ikiwa ni sehemu ya mpango mkubwa wa kuwaletea wananchi maendeleo.

Akizungumza leo kwenye tamasha la michezo ya jadi lililofanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage, Katambi amesema barabara nyingi ndani ya manispaa hiyo zitajengwa kwa kiwango cha lami, ikiwemo barabara ya kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga, ambayo kwa muda mrefu imekuwa kilio kwa wananchi.

Mbali na kuzungumza kwenye tamasha hilo, Katambi pia ametumia siku ya leo kutembelea kata 13 kati ya 17 za Jimbo lake la Shinyanga Mjini, ambapo amekutana na wananchi na kuzungumza nao kuhusu miradi mbalimbali ya maendeleo. Katika kila kata aliyotembelea, Katambi ametoa zaidi ya shilingi milioni tatu kwa ajili ya kutatua changamoto, ikiwa ni hatua ya haraka ya kuharakisha utekelezaji wa miradi midogo ya maendeleo.

“Tunaendelea kuwahudumia wananchi kwa vitendo. Hatuahidi tu bali tunatoa fedha kusaidia miradi kwenye kila kata. Kazi yetu ni kuhakikisha kuwa Shinyanga inabadilika kwa kasi,” amesema Katambi.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, amempongeza Mhe. Katambi kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye jimbo lake, huku akimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuonesha nia ya dhati ya kupeleka maendeleo kwa wananchi wa Shinyanga.

“Tunajivunia kuwa na Mbunge Katambi. Amekuwa kiongozi wa vitendo, na tumeshuhudia namna ambavyo Rais wetu Dkt. Samia amekuwa akivuta maendeleo kwa kasi isiyo na mfano. Tuna imani kubwa na Serikali ya Awamu ya Sita,” amesema Mlolwa.

Aidha, Mlolwa amewaomba wananchi waendelee kukiunga mkono Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kuwa kimeendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi mkubwa.

Tamasha hilo la michezo ya jadi limeibua hisia mbalimbali kutoka kwa wakazi wa Manispaa ya Shinyanga, ambapo wengi wamesema ni ishara kuwa viongozi wao hawawasahau bali wanajitahidi kurudi kwao na kusikiliza kero zao moja kwa moja.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Paschal Katambi, akizungumza kwenye tamasha la michezo ya jadi lililofanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage leo Mei 16, 2025.

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Paschal Katambi, akizungumza kwenye tamasha la michezo ya jadi lililofanyika katika Uwanja wa CCM Kambarage leo Mei 16, 2025.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Mabala Mlolwa, akimpongeza Mhe. Katambi kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye jimbo lake.








Post a Comment

Previous Post Next Post