Na Mapuli Kitina Misalaba
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, amesema kukamilika
kwa miradi mbalimbali ya maendeleo nchini kutaongeza kasi ya ukuaji wa uchumi wa
wananchi na Taifa kwa ujumla.
Ametoa kauli hiyo Mei 2, 2025, wakati wa ziara ya kukagua miradi
ya maendeleo inayotekelezwa Jijini Mwanza, ambapo amepongeza hatua nzuri
zilizofikiwa katika utekelezaji wa miradi hiyo huku akitoa wito kwa wakandarasi
kuendelea kufanya kazi kwa weledi, uadilifu na kwa kuzingatia muda.
Katika ziara hiyo, Msigwa
ametembelea na kukagua miradi mitatu muhimu ambayo ni: ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza, daraja la Busisi-kigongo ambalo limefikia
asilimia 99 ya ujenzi, pamoja na ujenzi
wa vivuko vipya vitano vinavyojengwa katika yadi ya Songoro Marine
Transport Limited jijini Mwanza.
Miongoni mwa miradi mikubwa inayotekelezwa
ukanda wa Ziwa Victoria ni ujenzi wa meli
mpya ya MV Mwanza, unaotekelezwa kwa ubia kati ya kampuni za Gas Entec na Kangnam Corporation zote kutoka Korea Kusini kwa kushirikiana na
SUMA JKT ya Tanzania.
Mradi huo ulianza kutekelezwa
Januari 17, 2019 na hadi sasa umefikia asilimia 98 ya utekelezaji wake. Gharama
za mradi zinakadiriwa kufikia Dola za Kimarekani 51,830,440.28 sawa na Shilingi
Bilioni 138.9. Hadi sasa Serikali tayari imelipa Dola za Kimarekani
48,899,790.26 (asilimia 94.35 ya gharama zote), sawa na Shilingi Bilioni 131.1.
Meli hiyo itakapokamilika, itakuwa
na uwezo wa kubeba abiria 1,200, mizigo ya tani 400, magari
madogo 20 na malori matatu. Itakuwa na madaraja sita ya abiria:
Economy (abiria 834), Business Class (200), Second Sleeping (100), First Class
(60), Executive (4) na VIP Class (2).
Meli hiyo itafanya safari kati ya
Mwanza, Bukoba, Musoma kupitia Kemondo Bay pamoja na nchi jirani za Uganda na
Kenya, hivyo kuimarisha biashara, usafirishaji na mahusiano ya kikanda.
Kwa sasa kazi iliyosalia ni ufungaji wa viti na samani, ambapo
kontena tisa za viti tayari zimeshawasili na mzigo wa mwisho wa samani za
vyumba vya kulala unatarajiwa kuwasili katikati ya mwezi Mei.
Wizara kupitia Wakala wa Ufundi na
Umeme (TEMESA) inaendelea na utekelezaji wa ujenzi wa vivuko vipya vitano
pamoja na ukarabati wa vivuko vitatu katika Kanda ya Ziwa.
Mradi huo unatekelezwa na Songoro Marine Transport Limited ya
jijini Mwanza na unalenga kutoa huduma katika maeneo ya Bwiro – Bukondo
(Ukerewe), Ijinga – Kahangala (Magu), Kisorya – Rugezi (Ukerewe), Nyakaliro –
Kome (Sengerema) na Buyagu – Mbalika (Sengerema/Misungwi).
Gharama za utekelezaji wa miradi hii
ni Shilingi Bilioni 18.6 pamoja na Dola za Kimarekani Milioni 3.79. Hadi sasa
Serikali imelipa kiasi cha Shilingi Bilioni 21.7 sawa na asilimia 75 ya madai
ya mkandarasi.
Usimamizi wa miradi hiyo unafanywa
na Mtaalam Mshauri kutoka DMI pamoja na udhibiti wa Shirika la Uwakala wa Meli
Tanzania (TASAC), ili kuhakikisha ubora na viwango vinazingatiwa kikamilifu.
Katika hatua nyingine, daraja la
Busisi-kigongo limefikia asilimia 99 ya ujenzi. Daraja hilo linatarajiwa kuwa
kiungo muhimu kati ya mikoa ya Mwanza na Geita, na hivyo kupunguza utegemezi wa
vivuko na kuboresha mzunguko wa shughuli za kiuchumi kati ya mikoa hiyo.
Msigwa amewataka wakandarasi kote
nchini kuendelea kutekeleza miradi kwa ubora na kwa muda uliopangwa, huku
akiwakumbusha wananchi kulinda miradi hiyo mara baada ya kukamilika.
“Serikali itaendelea kushirikiana na
wakandarasi wanaotekeleza miradi kwa weledi. Lakini pia, wananchi tunapaswa
kuitunza miundombinu hii kwa sababu ni ya kwetu wote,” amesema Msingwa.
Ameongeza kuwa uwepo wa miradi hiyo
utasaidia kuchochea mzunguko wa fedha, kupunguza gharama za usafiri, na
kuongeza kasi ya ukuaji wa sekta kama utalii, biashara, na usafirishaji katika
maeneo yote ya Ziwa Victoria.
Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu
Msigwa aliambatana na waandishi wa habari kutoka Shinyanga na Mwanza ambao
wameeleza kufurahishwa na hatua za utekelezaji wa miradi hiyo na kuahidi
kuendelea kuripoti kwa weledi baada ya kujionea maendeleo kwa macho yao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa akisaini
kwenye kitabu cha wageni baada ya kuwasili kwa ajili ya kutembelea Vivuko
vinavyojengwa Jijini Mwanza.

Mkurugenzi wa uendeshaji na ujenzi
wa vivuko atoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa akizungumza
baada ya kupokea taarifa ya mradi huo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakitembelea Vivuko vinavyojengwa Jijini Mwanza

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakitembelea Vivuko vinavyojengwa Jijini Mwanza


Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakitembelea Vivuko vinavyojengwa Jijini Mwanza

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakitembelea Vivuko vinavyojengwa Jijini Mwanza

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakitembelea Vivuko vinavyojengwa Jijini Mwanza

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakitembelea Vivuko vinavyojengwa Jijini Mwanza

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa
akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea Vivuko vitano
vinavyojengwa Jijini Mwanza.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa
akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea Vivuko vitano
vinavyojengwa Jijini Mwanza.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa
akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutembelea Daraja na Kigongo –
Busisi







Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakiwa katika Meli Mpya ya MV Mwanza.




Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa na
waandishi wa habari wakiwa katika Meli Mpya ya MV Mwanza.




Post a Comment