

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akimkabidhi cheti kwa Steve Kanyefu wa Gold FM, kama Mtangazaji Bora kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani – Mei Mosi 2025.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha akimkabidhi cheti kwa Emmanuel Mlelekwa wa Gold FM, kama Mwandaaji Bora wa Vipindi katika maadhimisho ya Mei Mosi 2025.
Na Mapuli Kitina Misalaba
Wafanyakazi wa Kituo cha Redio cha GOLD FM kilichopo
Wilayani Kahama, Mkoa wa Shinyanga wameibuka kidedea katika maadhimisho ya Siku
ya Wafanyakazi Duniani, Mei Mosi, baada ya kutunukiwa vyeti na zawadi za Laptop
kwa kutambua mchango wao katika tasnia ya utangazaji.
Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na Usafirishaji (Communication and Transport Workers
Union) COTWU imewatuza wafanyakazi hao kwa kazi nzuri na ubunifu mkubwa
waliouonesha katika uandaaji wa vipindi pamoja na utangazaji wenye weledi na
mvuto kwa jamii.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Anamringi Macha,
ndiye aliyekabidhi vyeti hivyo wakati wa maadhimisho hayo, ambapo Mtangazaji
Steve Kanyefu ametunukiwa Cheti cha Mtangazaji Bora, huku Emmanuel Mlelekwa
akikabidhiwa Cheti cha Mwandaaji Bora wa Vipindi.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka COTWU, zawadi za Laptop
tayari zimewasilishwa kwa Uongozi wa Gold FM ili zikabidhiwe rasmi kwa wahusika
hao waliong’ara.
Hatua hiyo imetajwa kuwa chachu ya kuongeza ari na
ubunifu kwa wafanyakazi katika sekta ya utangazaji huku ikitambua mchango wa
vyombo vya habari katika maendeleo ya jamii.
Gold FM Tanzania,
chombo cha habari kinachozidi kung'ara kanda ya ziwa na mikoa jirani,
hupeperusha matangazo yake kupitia masafa yafuatayo:
📻 88.7 Kahama
📻 88.7 Shinyanga
📻 94.5 Geita
📻 90.7 Simiyu
📻 94.5 Mwanza
📻 102.5 Tabora
📻 106.5 Kagera
📻 88.5 Mara
📻 102.1 Kigoma
Kupitia masafa haya, Gold FM imekuwa daraja la
taarifa, burudani na elimu kwa mamilioni ya wasikilizaji nchini Tanzania –
ikitangaza kwa weledi na ubunifu unaotambulika hadi ngazi za kitaifa kama
ilivyoonekana katika maadhimisho ya Mei Mosi mwaka huu.
Steve Kanyefu (Mtangazaji Bora) na Emmanuel Mlelekwa (Mwandaaji Bora wa Vipindi) wa Gold FM.






Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe.
Anamringi Macha akipongeza kituo cha Redio Gold FM
kwa kuwa sehemu ya wadhamini wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani –
Mei Mosi 2025, yaliyofanyika kimkoa na kwamba Mhe. Macha amesema mchango wa
Gold FM katika kuelimisha, kuhamasisha na kushirikiana na jamii ni wa kuigwa.
Post a Comment