" ZIARA YA U.W.T WILAYA YA SHINYANGA MJINI - UMOJA NA MSHIKAMANO IENDELEE KUWA SILAHA YA USHINDI

ZIARA YA U.W.T WILAYA YA SHINYANGA MJINI - UMOJA NA MSHIKAMANO IENDELEE KUWA SILAHA YA USHINDI

Viongozi wa umoja wa wanawake wa Tanzania  U.W.T  Wilaya ya Shinyanga Mjini wameanza ziara kwenye kata zote kuimarisha uhai wa wanachama wake

Katika siku ya kwanza ya ziara yao,viongozi hao wa U.W.T wamezungumza na wanachama wa jumuiya hiyo katika kata ya Ibadakuli manispaa ya Shintanga ambapo wamehamasisha zaidi kuhusu uhai wa wanachama na jumuiya zake, na kulipa ada kama inavyoelekezwa 

Akizungumza katika mkutano uliojumuisha viongozi ngazi ya  kata na matawii,pamoja na wenyeviti na wajumbe wa mitaa,vijiji na vitongoji   wa kata hiyo, mwenyekiti wa U.W.T wilaya ya Shinyanga mjini Bi Rehema Nhamanilo amewataka kuendeleza umoja na mshikamano,kuwajibikia  majukumu yao kwa weredi,ikiwa ni pamoja na kufanya vikao vya kikanuni, ili kukiimarisha chama na jumuiya zake

Mama Nhamanilo ameonya viongozi hao kuepuka makundi yasiyokuwa na tija hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais,wabunge na madiwani,kwa kuwa yanaweza kusababisha mpasuko ndani ya chama.

Mwenyekiti huyo amesisitiza viongozi hao kuwa chachu ya  umoja na mshikamano zaidi miongoni mwao  na kuepuka makundi yasiyokuwa na tija.

Amewakumbusha kuendelea kuwapa ushirikiano wabunge na madiwani waliopo madarakani,ili kuwatia moyo waweze kukamilisha majuku yaliyo mbele yao.

kwa upande wake katibu wa U.W.T  ( CCM) wilaya ya Shinyanga mjini Getrude Mboyi amesisitiza zaidi kuhusu uhai wa  jumuiya hiyo na,ambapo amehamasisha kusimamia  ulipaji wa ada,na kusajili wanachama wapya.

Maadili,kupinga ukatili wa kijinsia, na wanawake kujitokeza kwa wingi kugombea katika nafasi za uongozi ni kati ya mada zilizowasilishwa na viongozi hao wa U.W.T wilaya ya Shinyanga mjini.

ziara hiyo iliyoanza Mei 12, 2025 inaendelea leo katika kata za Kizumbi na Ibinzamata.

MWISHO

mwenyekiti wa U.W.T wilaya ya Shinyanga mjini Bi Rehema Nhamanilo 

 


 

Post a Comment

Previous Post Next Post