Na Mapuli Kitina Misalaba
Mbunge wa
Viti Maalum Mkoa wa Shinyanga kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Salome Makamba, leo Juni 29, 2025, amechukua rasmi fomu ya
kuwania nafasi hiyo kwa mara nyingine, kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).
Makamba
amekabidhiwa fomu hiyo na Katibu wa UWT
Mkoa wa Shinyanga, Bi. Habiba
Musimu, katika ofisi za chama hicho mkoani humo.
Akizungumza
mara baada ya kupokea fomu, Salome amesema anaingia tena katika mchakato huo
akiwa na nia thabiti ya kuendeleza
mapambano ya maendeleo ya wanawake wa Mkoa wa Shinyanga kwa moyo wa
uzalendo na kujitoa.
“Nina
uzoefu, dhamira ya kweli na moyo wa kujitoa kwa ajili ya maendeleo ya wanawake.
Niko tayari kuendelea kuwatumikia kwa heshima kubwa,” amesema Makamba.
Mbunge
huyo amesema kipindi chake cha awali kimemjengea uzoefu mkubwa katika kutetea
haki na fursa za wanawake, na anaamini kuwa bado ana nafasi ya kuchangia zaidi
maendeleo ya jamii hiyo, endapo atapewa ridhaa na chama.
Aidha Salome Makamba wakati anawasili ofisi hizo
ameingia kwa kutumia baiskeli
badala ya gari, akisema ni njia ya kuenzi na kudumisha asili ya maisha ya watu
wa Shinyanga.
Ameeleza kuwa aliamua
kutumia baiskeli kama njia ya kuonyesha mshikamano na wananchi wa kawaida, hasa
wanawake na vijana wanaotegemea usafiri wa baiskeli katika shughuli zao za kila
siku.




🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment