" JOHN STEPHANO LUHENDE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA BUKENE – NZEGA

JOHN STEPHANO LUHENDE ACHUKUA FOMU YA KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA BUKENE – NZEGA

Na. Elias Gamaya Nzega Tabora

 Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mkurugenzi wa Shirika la Luhende John Foundation lenye makao yake makuu Wilaya ya Nzega, mkoani Tabora, Ndg. John Stephano Luhende amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge wa Jimbo la Bukene kupitia CCM.

 Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu hiyo, Ndg. Luhende amesema kuwa uamuzi wake umetokana na nia ya dhati ya kuleta mabadiliko chanya katika jimbo hilo, kwa kushirikiana na wananchi kusukuma mbele gurudumu la maendeleo.

 “Nimeshawishika kuchukua fomu ya kuomba ridhaa kwa wananchi wa Bukene ili tufanye mabadiliko na kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Nina imani kuwa kwa kushirikiana na wananchi, tunaweza kulijenga upya jimbo letu,” amesema Ndg. Luhende.




 

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post