" MCHUNGAJI TAMBIKENI AWAHIMIZA WAUMINI T.A.G FOREST YA KWANZA MBEYA KUTOKATA TAMAA

MCHUNGAJI TAMBIKENI AWAHIMIZA WAUMINI T.A.G FOREST YA KWANZA MBEYA KUTOKATA TAMAA

Na Lydia LugakilaMbeya

Waumini wa kanisa la Tanzania assemblies of God (TAG) Mbeya Forest ya kwanza  wamehimizwa kutokata tamaa katika maisha badala yake wajikite katika ibada na kumcha Mungu.

Akiongoza ibada hiyo iliyofanyika kanisani hapo Agosti 31,2025 mtumishi wa Mungu Mchungaji Thobias Tambikeni ameeleza athari za kukata tamaa na kuwa hali hiyo inawatokea waumini pale majibu yanapochelewa.

Mchg Tambikeni amesema kuwa kukata tamaa ni mbaya kwani hali hiyo husababisha mashabulizi kuwa mepesi muno kwani adui shetani anapenya kwa haraka ambapo pia amewataka waumini hao kutambua kuwa Ile kazi ya uumbaji Mungu angeikatia tamaa uumbaji huo ungeishia hapo.

Akitaja Athari nyingine za kukata tamaa mtumishi huyo amesema kuwa ni kuangamia kabisa kiroho na kimwili, hivyo licha ya waumini hao kukutana na misukosuko mingi inayokatisha tamaa  hawatakiwi kukata tamaa kabisa.

Mtumishi huyo amesema kuwa waumini hao wanatakiwa kusimamia na yesu mpaka atokee ikiwa ni pamoja na kufurahi katika Bwana siku zote pale unapookoka na  haijalishi upo mazingira gani.

Akitaja Dalili za kukata tamaa amesema kuwa mtu aliyekata tamaa ujitenga na wengine, hujikatia tamaa na kujichukia au kujinyanyapaa mwenyewe akidhani anasemwa na wengine.

"Dalili nyingine za kukata tamaa ni kuwa na manunguniko na lawama, kutokutamani ushauri" alisema mtumishi huyo.

Aidha amesema Mungu hajawahi kushindwa wala kuchoka hivyo ni wakati wa kuinuka.

Amesema kuwa hali ya kukata tamaa imelitesa kanisa la sasa hivyo waumini wanatakiwa kutambua kuwa Bwana Yesu analeta matumaini na faraja kwa haraka.

Mchungaji Tambikeni amewahimiza waumini hao kujipa moyo  kwani kazi ya Bwana ni kuleta matumaini.

Amewaomba waumini hao kumfanyia Mungu ibada na kutokubakia nyumbani kwani madhara yake  ni hatari sana.

Amesema ukitii Bwana anajitokeza kwa mazingira usiyodhani na kutenda muujiza hivyo safari ya kusonga mbele inahitaji nguvu ya Mungu kwani bado kuna vita na mapambano.

Hata hivyo amewashauri waumini  kumfanyia Mungu ibada kwani matumaini ya mtu  yanapotea pale mtu unapoonyesha dalili za kukata tamaa hivyo wasilie wala wasichoke maana katika mazingira hayo shetani huwapitia.

Post a Comment

Previous Post Next Post