
Na Lydia Lugakila, Misalaba Media
"Bado Mwandemba hajashika wadhifa huo wa udiwani
huo lakini tayari ameisha omba Barabara za kata ya Nsalaga kupitia vikao vikuu.
"Nawashukuru wajumbe walifanya jambo jema
kutuletea kijana Mwandemba (dogo Janja) kwani Halmashauri ya Jiji la
Mbeya inakwenda kuwa diwani mdogo hakika wamechagua maendeleo" alisema Mwaiteleke.
Naye katibu wa Taasisi ya Mtetezi wa Mama Mkoa wa
Mbeya Boazi Mwasongole amesema kuwa Mwandemba amekuwa Mwenyekiti wa umoja wa
vijana (UVCCM) Mbeya mjini hakuweza kuwaacha vijana wa kata ya Nsalaga kwa
Fursa mbali mbali za kiuchumi huku akiwaomba kuweka kura nyingi kwa Dokta Tulia
kutokana na kuliheshimisha Taifa kwa uongozi imara.
"Sisi madreva bajaji alitusaidia kipindi cha mvua
leo ameomba Barabara za Nsalaga ni jambo jema kwetu kwani Nsalaga tunahitaji kupata mtu sahihi Kama
huyu"alisema Kayala.
Naye Mgombea udiwani kata ya Mwasanga Brandy Nelson
Mwinuka amesema kuwa kila mtu anajua ni jinsi gani chama cha mapinduzi(CCM)
kimefanya kazi kubwa hivyo wakichague kwa kishindo ili kiwaletee maendeleo.
"Nsalanga mmepata jembe maana Mwandemba ni kijana
ambaye anaweza kupitia sehemu hata zisizopitika hivyo tumchague ili aibadili kata yetu"alisema
Mwinuka.

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment