" SMAUJATA SHINYANGA YAWAALIKA WANANCHI KUCHANGIA DAMU SALAMA NA KUPIMA AFYA

SMAUJATA SHINYANGA YAWAALIKA WANANCHI KUCHANGIA DAMU SALAMA NA KUPIMA AFYA

Jumuiya ya Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania (SMAUJATA) Mkoa wa Shinyanga inawaalika wananchi wote wa mkoa huo kushiriki katika zoezi la kuchangia damu salama kwa lengo la kuokoa maisha ya watu wenye uhitaji.

Akizungumza Mwenyekiti wa SMAUJATA Mkoa wa Shinyanga Nabila Kisendi amesema kampeni hiyo inalenga kuhamasisha mshikamano wa kijamii kwa kuhakikisha hospitali zinakuwa na hifadhi ya damu ya kutosha kwa ajili ya wahitaji.

Sambamba na kuchangia damu, wananchi watakaohudhuria watapata pia huduma za bure za kupima afya ikiwemo shinikizo la damu (pressure), kiwango cha sukari mwilini pamoja na magonjwa mengine ya hali ya maisha.

Huduma hizi zitatolewa kwa ushirikiano wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga kupitia ofisi ya Mganga Mfawidhi wa Mkoa.

SMAUJATA imewaomba wadau na wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika zoezi hilo, kwani kila tone la damu linalotolewa lina mchango mkubwa katika kuokoa maisha ya wagonjwa, hususan wajawazito, watoto, na wahanga wa ajali.

Zoezi la kuchangia damu linatarajiwa kufanyika siku ya Alhamisi wiki hii katika eneo la  stand ya Hiace karibu na soko kuu la Mkoa wa Shinyanga


 

🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA KAMPUNI YA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA

Post a Comment

Previous Post Next Post