Na Mapuli Kitina Misalaba
Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, viongozi wa
Jumuiya ya Wazazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka ngazi ya taifa na wilaya
ya Shinyanga Mjini wameendelea kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika
zoezi la kupiga kura, huku wakisisitiza umuhimu wa kudumisha amani, umoja na
uzalendo.
Ziara hiyo imefanyika leo Oktoba 6, 2025 katika soko
la Kambarage Mjini Shinyanga, ambapo viongozi hao wa jumuiya wamekutana na
wafanyabiashara na kuwataka kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi bora
kupitia CCM katika ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani ifikapo Oktoba 29, 2025.
Ujumbe wa viongozi hao kutoka makao makuu ya Jumuiya
ya Wazazi CCM Taifa umejumuisha Mkuu wa Idara ya Uchumi, Mipango na Fedha
Jamali Adam, Katibu Msaidizi Idara ya Utawala Eva Jeremiah, na Katibu Msaidizi
Idara ya Siasa na Uenezi Nanyaro Urassa, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jumuiya
ya Wazazi Wilaya ya Shinyanga, Mzee Fue Mrindoko, pamoja na Katibu wa Jumuiya
hiyo, Bi. Doris Kibabi.
Akizungumza katika mkutano huo, Jamali Adam amewahimiza
wafanyabiashara wa soko la Kambarage kuendelea kuwa wazalendo, kulinda amani na
utulivu wa nchi, huku wakijivunia maendeleo makubwa yaliyoletwa na Serikali ya
Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
“Amani ni tunu ambayo kila Mtanzania
anapaswa kuilinda. Serikali ya CCM imefanya kazi kubwa katika kuimarisha
uchumi, kuboresha huduma za kijamii na kuwakwamua wananchi kiuchumi. Ni wajibu
wetu kushiriki uchaguzi huu kwa amani na kuichagua tena CCM ili maendeleo haya
yaendelee,” amesema Jamali.
Kwa upande wake, Katibu Msaidizi Idara ya Siasa na
Uenezi Nanyaro Urassa amewasisitiza wafanyabiashara kupuuza watu wanaopotosha
au kujaribu kuleta mgawanyiko katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi,
akisisitiza kwamba Chama Cha Mapinduzi ndicho chenye dira na uongozi unaojali
wananchi.
“Tusikubali kurudishwa nyuma na maneno ya
siasa yasiyo na tija. Kura yako ina thamani kubwa, hakikisha unapiga kura kwa
CCM ili kuendelea kupata maendeleo,” amesema Urassa.
Naye Eva Jeremiah amewaomba wananchi kuhakikisha
wanashiriki kikamilifu siku ya uchaguzi na kuhamasisha ndugu na marafiki zao
kujitokeza kwa wingi.
“Tarehe 29 Oktoba ni siku muhimu. Twendeni
kwa amani, tupige kura kumchagua Rais Samia, wabunge na madiwani wote wa CCM.
Kila kura ni sauti ya maendeleo,” amesema Eva.
Aidha, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya
Shinyanga, Mzee Fue Mrindoko, pamoja na Katibu Bi. Doris Kibabi, wametumia
nafasi hiyo kuwaombea kura wagombea wa CCM, wakiwemo Rais Samia, mbunge wa
Shinyanga Mjini na mgombea udiwani wa Kata ya Kambarage, Hamis Haji Kabuta,
wakisisitiza kuwa ni viongozi wenye nia njema ya kuleta maendeleo kwa wananchi.
Kwa upande wake, Hamis Haji Kabuta, mgombea udiwani wa
Kata ya Kambarage kupitia CCM, ameahidi kwamba endapo atachaguliwa, ataboresha
miundombinu ya soko la Kambarage na maeneo ya biashara ili wafanyabiashara
wafanye kazi katika mazingira salama na ya usafi.
“Kipaumbele changu ni kuhakikisha soko la
Kambarage linakuwa la kisasa, lenye miundombinu bora na huduma za msingi
zinazostahili. Huu ni muda wa kuleta mageuzi ya kweli ya kimaendeleo,”
amesema Kabuta.
Wafanyabiashara wa soko hilo kwa upande wao
wamepongeza ujio wa viongozi wa Jumuiya ya Wazazi Taifa na kuahidi kujitokeza
kwa wingi siku ya kupiga kura, huku wakiahidi kuunga mkono wagombea wa CCM
katika ngazi zote.
Wakizungumza kwa niaba ya wenzao, baadhi ya
wafanyabiashara wameeleza kuwa wana imani kubwa na Serikali ya CCM kwa namna
inavyotekeleza miradi ya maendeleo, ikiwemo kuboresha huduma za jamii na
mazingira ya biashara.
Jumuiya ya wazazi CCM kupitia viongozi wake leo wamezungumza
na wafanyabiashara mbalimbali wakiwemo wauzaji wa matunda, mama lishe, wauzaji
wa kuku na nyama, mafundi seremala pamoja na waendesha bodaboda ambapo Jana,
msafara huo umetembelea Kata ya Chibe, Mjini, na kufanya mkutano wa hadhara
katika Kata ya Ibinzamata.
Ziara ya Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa inaendelea katika
maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Shinyanga, ikiwa na lengo la kuhamasisha wananchi
kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu ujao, kudumisha uzalendo, na kuendelea
kuiamini CCM kama chama kinacholeta maendeleo ya kweli kwa Watanzania.
Viongozi wa jumuiya ya Wazazi kutoka Taifa wakisaili kwenye kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika ofisi ya CCM kata ya Kambarage.

Viongozi wa jumuiya ya Wazazi kutoka Taifa wakisaili kwenye kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika ofisi ya CCM kata ya Kambarage.

Viongozi wa jumuiya ya Wazazi kutoka Taifa wakisaili kwenye kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika ofisi ya CCM kata ya Kambarage.


Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea
kuhamasisha wananchi kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea
kuhamasisha wananchi kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea
kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa
kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Kibabi akihamasisha wafanyabiashara
wa Kuku kujitokeza kupiga kura Oktoba 29, 2025.

Katibu wa Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Shinyanga
mjini Bi. Doris Kibabi akihamasisha wafanyabiashara
wa Kuku kujitokeza kupiga kura Oktoba 29, 2025.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Mgombea udiwani wa Kata ya Kambarage kupitia CCM, Hamis
Haji Kabuta, akiahidi kuboresha miundombinu ya soko la Kambarage.

Mgombea udiwani wa Kata ya Kambarage kupitia CCM, Hamis
Haji Kabuta, akiahidi kuboresha miundombinu ya soko la Kambarage.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi CCM Taifa wakiendelea kuhamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kushiriki kwa amani katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu.

Katibu Msaidizi Idara ya Siasa na Uenezi Nanyaro
Urassa akiwasisitiza wafanyabiashara kupuuza watu wanaopotosha au kujaribu
kuleta mgawanyiko katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.

Katibu Msaidizi Idara ya Siasa na Uenezi Nanyaro
Urassa akiwasisitiza wafanyabiashara kupuuza watu wanaopotosha au kujaribu
kuleta mgawanyiko katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi.


Mkuu wa Idara ya Uchumi, Mipango na Fedha Jamali Adam,
akiwahamasisha wafanyabiashara wa soko la Kambarage kutumia haki yao ya kikatiba kuchagua viongozi
bora kupitia CCM katika ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani ifikapo Oktoba 29,
2025.

Mgombea udiwani wa Kata ya Kambarage kupitia CCM, Hamis
Haji Kabuta, akiahidi kuboresha miundombinu ya soko la Kambarage.

Mgombea udiwani wa Kata ya Kambarage kupitia CCM, Hamis
Haji Kabuta, akiahidi kuboresha miundombinu ya soko la Kambarage.

Mjumbe wa kamati ya utekelezaji wa jumuiya ya Wazazi
CCM Wilaya ya Shinyanga mjini Bi. Zulfa Hassan akiwa na Katibu Msaidizi Idara
ya Utawala Eva Jeremiah.
🥃🍶 TUMIA VINYWAJI BORA VYA EAST AFRICAN SPIRITS – BEI RAFIKI, LADHA SAFI BILA HARUFU MBAYA
Post a Comment