Waziri Mkuu wa zamani Nchini Kenya, Raila Odinga amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 80.
Amefariki dunia Jumatano wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja nchini India.
Kifo chake kinakuja kufuatia tetesi zilizodai kuwa alikuwa katika hali mahututi.
Awali, familia yake ilikuwa imejitokeza na kukanusha vikali uvumi huo, ikisisitiza kuwa alikuwa na hali nzuri na alikuwa akiendelea kupona vizuri.
Kaka yake mkubwa ambaye pia ni Seneta wa Siaya, Oburu Odinga, aliwahakikishia Wakenya kwamba kiongozi wa ODM alikuwa na afya njema na alikuwa akipata nafuu nchini India baada ya kuumwa kidogo.
Akizungumza na vyombo vya habari, Oburu alikanusha taarifa zilizodai kwamba Raila alikuwa katika hali mbaya, akizitaja kuwa zimezidishwa na si sahihi.
Post a Comment